Posts

Showing posts from March, 2015

IDADI YA WALIOKUFA MAAFA YA MAFURIKO KAHAMA YAFIKIA 47

Image
IDADI ya watu waliofariki kutokana na mvua kubwa ya mawe, iliyopewa jina la tonado, sasa imefikia watu 47 baada ya majeruhi mwingine aliyekuwa amelazwa katika hospitali ya wilaya ya Kahama kufariki dunia juzi. Taarifa ya ongezeko la vifo imetolewa jana na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Dk Ally Rufunga alipokuwa akipokea misaada ya waathirika wa maafa hayo kutoka kwa watu mbalimbali, akiwemo Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, Freeman Mbowe na mwakilishi wa Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa. Pia Rufunga alipokea misaada kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Issa Machibya ambaye alikabidhi vyakula na mafuta ya kula aina ya mawese lita 400, sabuni za kufulia katoni 32, chumvi kilo 357, dagaa gunia 12, mchele kilo 200 na maharage kilo 815. Vitu hivyo vilitolewa na wakazi wa mkoa wa Kigoma wa ajili ya kuwasaidia waathirika hao. Akikabidhi msaada kwa niaba ya familia ya Lowassa, Mwenyekiti wa CCM mkoani Shinyanga, Khamis Mgeja alisema baada ya kutokea kwa maafa

JAMANI JAMANI KUMBE KIZIMBANI PACHUNGU HIVI.....MTUHUMIWA HUYU WA ESCROW AJICHANGANYA

Image
MKURUGENZI Mdhibiti Uchumi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA), Dk James Diu, amejichanganya mbele ya Baraza la Maadili ya Viongozi wa Umma, kuhusu matumizi halisi ya fedha alizozipokea kutoka kwa James Rugemalira ambazo ni Sh milioni 80.8. Akijitetea mbele ya baraza hilo, Mkurugenzi huyo ambaye pia aliwahi kushika wadhifa wa Meneja Udhibiti Uchumi katika Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA), alikiri kupokea kiasi hicho cha fedha ambacho alidai alikitumia kwa ajili ya matibabu ya mkewe aliyefariki dunia Agosti mwaka jana kwa ugonjwa wa saratani. Hata hivyo, katika maelezo yake aliyoyatoa mbele ya Kamati ya Uchunguzi ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma na tamko lake la mali na madeni alilolitoa Desemba 30, mwaka jana katika Sekretarieti hiyo, kiongozi huyo alibainisha kutumia kiasi hicho cha fedha katika kulipia deni lake la nyumba alilokuwa akidaiwa. Awali Wakili wa Sekretarieti hiyo ya maadili, Wemaeli Mtei, akimsomea mashtaka mku

Watu saba wanashikiliwa na Jeshi la polisi kwa tuhuma za kukata kiganja cha mtoto Albino Sumbawanga

Image
Jeshi la polisi mkoani rukwa linawashikilia watu saba hadi sasa, kwa tuhuma za kuhusika na kitendo cha kikatili cha kukata kiganja cha mkono wa kulia, cha mtoto mwenye ulemavu wa ngozi Baraka Cosmas Lusambo mwenye umri wa miaka sita, katika kitongoji cha kikonde kata ya kipeta wilaya ya sumbawanga vijijini, ambapo pia katika tukio hilo wamemjeruhi mtoto huyo mkono wa kushoto.   Kaimu kamanda wa polisi wa mkoa wa rukwa kamishna msaidizi wa polisi Leons Rwegasira, amesema wamefanikiwa kuwakamata watu hao kufuatia msako mkali, mara tu baada ya kutokea tukio hilo kwenye kitongoji hicho cha kikonde, ambacho kinakuwa na wakazi wakati wa msimu wa kilimo na kiangazi watu wanahama tena, katika familia yenye watoto wengine watatu wenye ulemavu wa ngozi.    ACP.Rwegasira pia amesema kwenye msako huo mkali, wamefanikiwa kuwakamata watu wanane wanaojihusisha na uganga wa jadi na upigaji wa ramli chonganishi, ambacho ni chanzo kikubwa cha kusababisha vifo na kujeruhiw

MWANAFUNZI WA SEKONDARI AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA ZA KUMUUA ASKARI WA JWTZ KWENYE MAPIGANO YA AMBONI TANGA

Image
WAKAZI 10 wa jijini hapa, akiwemo mwanafunzi wa sekondari wamefikishwa mbele ya Mahakama ya Hakimu Mkazi wakikabiliwa na makosa matano tofauti kuhusu tukio la kuwanyang’anya polisi silaha pamoja na kumuua askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Sajenti Mohamed Rashid Kajembe. Mwanafunzi aliyefikishwa mahakamani ni Rajab Bakari (19) wa shule ya sekondari na mkazi wa Makorora jijini hapa. Watuhumiwa tisa wameelezwa kuwa ni wafanyabiashara, nao ni Mbega Seif (25) maarufu ‘Abuu Rajab’ mkazi wa Kiomoni, Amboni, Ayubu Ramadhani (27) maarufu ‘Chiti’ ambaye ni fundi umeme na mkazi wa Kona Z Kiomoni, Hassani Mbogo (20) maarufu ‘Mpalestina’ mkazi wa Makorora, Mohamed Ramadhani (19) mfanyabiashara na mkazi wa Makorora, Sadiki Mdoe (25) maarufu ‘Kizota au Kisaka’ mkazi Magaoni. Washtakiwa wengine ni Saidi Omari (26) mkazi wa Magaoni Tairi Tatu, Nurdin Mbogo (27) Makorora, Ramadhan Mohamed (18) mkazi wa Donge pamoja na Omari Harubu Abdala (55) maarufu

NEC yaongeza muda wa kujiandikisha Makambako mkoani Njombe

Image
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeongeza muda wa siku mbili zaidi katika zoezi la uandikishaji wapiga kura kwenye daftari lakudumu la wapiga kura kwa njia ya Biometric voters registration (BVR) lililokuwa limalizike hii leo katika halmashauri ya mji wa Makambako mkoani Njombe kutokana na idadi kubwa ya watu waliojitokeza kujiandikisha.   blog hii  ilifika katika baadhi ya vituo kwenye mitaa ya mji wa Makambako na kukuta misururu ya watu walio na shauku ya kujiandikisha katika daftari hilo ili kuwahi muda wa kufunga zoezi hilo huku baadhi yao wakieleza kuwa muda wa wiki moja kufanya zoezi hilo uliopangwa na tume ya taifa ya uchaguzi hautoshi kwani watu wengi hawajajiandikisha bado hadi leo.   Majira ya saa kumi jioni tulifika katika ofisi za halmashauri ya mji wa Makambako na kuzungumza na mkurugenzi wa halmashauri hiyo Bibi Vumilia Nyamoga ambaye ameeleza namna zoezi linavyoendelea na kutoa tangazo hilo la tume ya uchaguzi linaloeleza kuongezwa muda wa zoezi hilo na

RED BRIGADE WA CHADEMA, WALA KIAPO MBELE YA MBOWE, MWANZA

Image
Vijana wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, almaarufu kama RED BRIGADE, wakila kiapo cha utii, mbele ya Mwenyekiti wa taifa wa chama hicho, Freeman Mbowe, jijini Mwanza leo Jumamosi Februari 28, 2-015. Kiapo hicho kinafuatia kkamilika kwa mafunzo ya kiulinzi na usalama kwa vijana hao, ambapo nchi inaelekea kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu 2015. Vijana hao wakila kiapo mbele ya Mbowe, (kulia). Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa CHADEMA, Wilfred Rwakatare (kulia), kiasoma taarifa ya mafunzo ya vijana wa chama hicho 'Red Brigedi' huku mwenyekiti wa taifa wa chama hicho, Freeman Mbowe (kushoto) akisikiliza kwa makini. Vijana hao wakitoa heshima mbele ya Mwenyekiti wao Mbowe.PICHA KWA HISANI YA KIVIS BLOG

UTORO, MIMBA: CHUNYA NI ZAIDI YA KYELA

Image
WAZIRI MKUU Mizengo Pinda ameendelea kukemea tabia za utoro na mimba kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wilayani Chunya baada ya kupewa taarifa kwamba watoto 4,420 walitoroka shule na wengine 201 kupata mimba. Februari 26, mwaka huu, Waziri Mkuu aliwaagiza Mkuu wa Wilaya ya Kyela pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo kuwasaka na kuwakamata wale wote waliohusika na utoro na ujauzito wanafunzi na kuwafikisha mahakamani mara moja ili liwe fundisho kwa wengine baada ya kuelezwa kwamba wanafunzi 94 walipata ujauzito na wengine 645 kuacha shule kwa sababu ya utoro. Akizungumza na maelfu ya wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika jana (Jumamosi, Februari 28, 2015) kwenye uwanja wa Saba Saba wilayani Chunya, Waziri Mkuu alisema haiwezekani kuiacha hali hiyo iendelee huku watoto wa wilaya hiyo wakiharibiwa maisha kwa kukosa masomo. “Utoro kwenye shule za msingi, taarifa ya wilaya inaonyesha watoto 1,979 waliacha shule

Kapteni John Komba kuzikwa Mbinga, Jumanne Machi 3

Image
Mwili wa Mbunge wa jimbo la Mbinga Magharibi nchini Tanzania Kapteni mstaafu John Komba unatarajiwa kuagwa leo katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam. Akizungumza nyumbani kwa marehemu Komba. Mmoja wa watoto wake Gerard Komba amesema mara baada ya kuagwa kwa mwili huo hapo kesho utasafirishwa hadi katika kijiji cha Lituhi wilayani Mbinga tayari kwa maziko yatakayofanyika kesho kutwa siku ya Jumanne.   Rais Jakaya Kikwete ni miongoni mwa viongozi waliofika nyumbani kwa marehemu Komba leo, kuifariji familia ya marehemu akiambatana na mkewe Mama Salma Kikwete.    Akitokea mjini Dodoma akiwa ameambatana na viongozi mbalilmbali wa chama cha mapinduzi, pamoja na mkewe mama Salma Kikwete, Rais Kikwete ametia saini kitabu cha maombolezo na kisha kuzungumza na familia ya marehemu Kaptein John Komba mbunge wa Mbinga na kuzungumza na viongozi mbalimbali wa chama, serikali ndugu jamaa na marafiki waliofika nyumbani kwa marehemu maeneo ya Mbezi Tangibovu jijini

Wananchi Chunya walala chini wakiomba waziri mkuu kuigawa wilaya yao

Image
Waziri mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda ameahidi kuigawa wilaya ya Chunya ili kupata wilaya mbili kabla ya uchaguzi mkuu ujao unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu. Uamuzi wa waziri mkuu kuigawa wilaya ya Chunya haraka unatokana na maombi ya wananchi wa jimbo la Songwe hususan katika kijiji cha Buyuni ambao wameamua kulala chini kwenye mavumbi, huku mbunge wa jimbo la Songwe, Mheshimiwa Philip Mulugo akipiga magoti chini na kumwomba waziri mkuu kuigawa wilaya hiyo kwa madai kuwa ina maeneo makubwa kijiografia hali ambayo inakwamisha maendeleo ya wananchi.   Mkuu wa mkoa wa Mbeya akamweleza waziri mkuu kuwa ukubwa wa wilaya ya Chunya ni asilimia 46 ya ardhi yote ya mkoa wa Mbeya hivyo maombi ya wananchi hao yana hoja ya msingi, huku wa wilaya ya Chunya Deodatus Kinawiro akielezea uwezo wa halmashauri ya wialaya ya Chunya kiuchumi kuwa inajitegemea kwa asilimia 15.   Waziri mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda amesema kuwa kikwazo pekee cha kuig