Posts

Showing posts from November, 2015

"Hatujaridhia kumuachia Maalim Seif kutangazwa mshindi wa Zanzibar" yasema CCM

Image
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimekanusha taarifa iliyosambazwa kupitia mitandao ya kijamii ya kuridhia Mgombea wa Chama Cha (CUF) Maalim Seif Sharif Hamad atangazwe kuwa Rais wa Zanzibar.  Akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake Kisiwandui mjini hapa Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Zanzibar, Vuai Ali Vuai, alisema wamepokea kwa msikitiko makubwa taarifa hizo alizoziita za uzushi.  Alisema chama chake hakipo tayari kuvunja katiba wala sheria kwa kuridhia kuwa Maalim Seif atangazwe, kwani uchaguzi uliofanyika tayari umefutwa rasmi na Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) kupitia Gazeti la Serikali.  "Mtandao huo wa kijamii ulidai kuwa mimi Naibu Katibu Mkuu niliwataka wananchama na wananchi wote kuridhia hatua hiyo iliyofikiwa ya chama chetu kuridhia kuapishwa Maalim Seif, huku nikisisitiza kwa kuwataka wananchi wote wajitokeze kwa wingi katika sherehe za kuapishwa rais", alisema Vuai.  Aliongezea kusema, "mbali ya hayo pia tarifa hizo zilinisin

Baba akamatwa akimbaka binti yake huko Mara

Image
Jeshi la polisi wilayani bunda linamshikilia mwanaume mmoja kwa tuhuma za kumbaka binti yake wa kuzaa ambaye ni mwanafunzi wa shule ya msingi Afisa tarafa ya chamriho, bw. Boniphace maiga, amemtaja mwanaume huyo kuwa ni athuman jeck mkazi wa kijiji cha mariwanda, kata ya hunyari wilayani hapa. Amesema kuwa mwanaume huyo alimfanyia unyama huo binti yake wakati mke wake akiwa amekwenda kwenye biashara, zake ambapo anadaiwa kumfungia ndani ya nyumba yao na kuanza kumbaka. Baada ya kitendo hicho binti huyo alikwenda kumwambia mama yake mzazi huku akitokwa na damu sehemu zake za siri Mtuhumiwa huyo atafikishwa mahakamani uchunguzi utakapokamilika

Watu wanne wahukumiwa jela miaka 32 Nzega

Image
Mahakama ya hakimu mkazi wilaya ya nzega imewahukumu kifungo cha miaka 32 jela watu nane kwa kosa la kufanya uvamizi na kuiba dhahabu tofali sita na nusu zenye thamani ya zaidi ya hsilingi bilioni 4 katika mgodi wa dhahabu wa resolute Akitoa hukumu hiyo hakimu mkazi silyvester kainda amesema washitakiwa mawazo saliboko ,edward bunera ,shaaban amuru,john ndaki,pius shija ,aloyce zindoro ,davidi ndaki pamoja na frenk kabuche wamehukumiwa kwenda jela miaka 30 baada kutiwa hatiani kwa makosa mawili makosa hayo ni kula njama za kufanya uhalifu katika mgodi wa dhahabu wa resolute ambalo wamehukumiwa kwenda jela miaka miwili kila mmoja pamoja na kosa la pili kufanya uhalifu kwa kutumia silaha ambapo ambalo wamehukumiwa kwenda jela miaka 30 kila mmoja. Watuhumiwa hao walikuwa wakikabiliwa na makosa 16 likiwepo kosa la kula njama ya kufanya uhalifu,kufanya uhalifu kwa kutumia silaha na utakatishaji pesa haramu. Akisoma mashitaka hayo mwanasheria wa seri

Zoezi la bomoa bomoa lapiga hodi Kahama

Image
Zoezi la bomoa bomoa linaloendelea nchini kwa kubomoa nyumba zilizojengwa kwenye maeneo ya wazi limeingia wilayani Kahama kwa hatua ya kwanza ambayo itazikumba kata za Kahama Mjini, Majengo, Nyahanga, Nyasubi na Nyihogo. Hayo yameelezwa leo na Mkurugenzi wa Halmashauri ya mji wa Kahama Anderson Msumba ambaye amesema kwa kuanza katika Kata hizo tayari viwanja 48, wamiliki wake amewataka wawasilishe ofisini kwake nyaraka za kumiliki maeneo hayo. Msumba amesema baada ya zoezi hilo la kuwasilisha nyaraka za umiliki wa maeneo hayo zitachunguzwa upatikanaji wake na hati miliki zitapelekwa kwa Waziri mwenye dhamana kwa ajili ya kufutwa na baadaye zoezi la kubomoa litaanza kwa maeneo hayo. Ameagiza umiliki wa maeneo ya hoteli za CDT na zahanati ya Community Health Dispensary uchunguzwe na hatua za ubomoaji ziendelee ikithibitika madai kuwa maeneo hayo ni ya wazi. Kwa mujibu wa Mkuu wa Idara ya Ardhi na Maliasili katika Halmashauri hiyo Joachim Henjewele, tayari kikosi chake c

Umeipata hii kesi ya TB Joshua mahakamani?

Image
Mchungaji wa Kanisa la Church of All Nations Nigeria, TB Joshua na Wakandarasi wawili ambao wanakabiliwa na mashtaka ya uzembe uliopelekea jengo la Kanisa hilo kuanguka na kusababisha vifo vya watu 116, leo wameshindwa kufika Mahakamani kusikiliza kesi inayowakabili kuhusu vifo vya watu hao. Kesi hiyo ilifunguliwa Mahakama Kuu ya Lagos Nigeria baada ya tukio la kuanguka kwa jengo la kufikia wageni lililopo kwenye Kanisa la TB Joshua September 12 2014 na kupelekea vifo hivyo ambapo kati ya waliofariki, 81 walikuwa raia wa Afrika Kusini. Katika Mashtaka yaliyofunguliwa Mahakamani, Kanisa hilo limedaiwa kufanya ujenzi wa jengo hilo la ghorofa sita bila kuwa na kibali cha kufanya ujenzi huo. Kwa upande wa TB Joshua wamekuwa wakijitetea kwamba sababu ya jengo hilo kuanguka inatokana na ndege moja ambayo ilizunguka juu ya jengo hilo, muda mfupi baadae jengo hilo likaanguka.. anaamini kuna hujuma zilizofanywa kwenye tukio hilo. Kukosekana kwa T B Joshua na wakandarasi hao kumela

Picha 37 za ziara ya Mkuu wa wilaya alivyokutana na vyoo vya ajabu ziko hapa

Image
Hiki choo cha ajabu kiko Shinyanga maelezo yapo chini.Leo Jumatatu Novemba 30,2015 ambapo mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro ameanza kufanya ziara kutembelea kata za manispaa hiyo ili kuangalia hali ya usafi wa mazingira kubwa zaidi ni kukagua vyoo vya wananchi ilimkukabiliana na ugonjwa wa kipindupindu. Mkuu huyo wa wilaya ya Shinyanga alikuwa ameambatana na mkurugenzi wa manispaa ya Shinyanga Lewis Kalinjuna,mwanasheria wa manispaa hiyo Simon Jilanga,afisa afya wa manispaa hiyo Heri Nakuzelwa,waandishi wa habari na askari wa jeshi la polisi. Mkuu huyo wa wilaya ametembelea kata ya Chibe na Kambarage na kubaini kuwa kaya nyingi hazina vyoo na kuagiza wajenge vyoo haraka huku akifunga maduka matano kutokana na kukosa vyoo. Mwandishi,Kadama Malunde alikuwepo kwenye msafara huo ametusogezea picha 37 kilichojiri.... Ziara ilianzia katika ofisi ya afisa mtendaji wa kata ya Chibe katika manispaa ya Shinyanga.Pichani ni mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephin

Kamanda Alphonce Mawazo azikwa...angalia picha zote hapa

Image
Mwenyekiti wa taifa wa chama cha demokrasia na maendeleo (Chadema) Mh. Freeman Mbowe ameongoza mamia ya wakazi wa mkoa wa Geita katika mazishi ya aliyekuwa mwenyekiti wa chama hicho mkoani humo Alphonce Mawazo yaliyofanyika leo kijijini kwao Chikobe wilayani Geita. Mazishi hayo yalitanguliwa na waombolezaji kutoa heshima zao za mwisho katika uwanja wa kijiji cha Chikobe licha ya mvua kubwa iliyokuwa ikinyesha kuanzia majira ya asubuhi. Viongozi wengine waliohudhuria mazishi hayo ni pamoja na aliyekuwa mgombea urais wa Chadema akiungwa mkono na vyama vinavyounda umoja wa katiba ya wananchi (UKAWA) Mh. Edward Lowassa, waziri mkuu mstaafu wa serikali ya awamu ya tatu Mh. Fredrick Sumaye, makamu mwenyekiti wa Chadema upande wa Zanzibar Said Issa Mohamed na kaimu katibu mkuu wa Chadema Salum Mwalimu. Ilipotimu majira ya saa tisa na dakika ishirini na moja alasiri jeneza lililoubeba mwili wa marehemu Alphonce Mawazo likashushwa kaburini na vijana wa kikosi cha ulinz

Wingu lilivyowafungia wachina ndani kwa muda wa siku tatu…

Image
Headlines zimerudi China..mamlaka ya hali ya hewa imetoa tahadhari kwa watu kutoka nje baada ya kutokea uchafuzi wa mazingira ulioukumba mji mkuu wa nchini hiyo Beijing. Mji huo ambao umekuwa katika hali ya tahadhari tangu mwanzoni mwa mwaka huu unasemekana kukumbwa na wingu zito baada ya mkaa kuwashwa maeneo mbalimbali kukabiliana na baridi kali. Baadhi ya mitaa ya Beijing ikiwa imekumbwa na wingu zito Serikali ya China imetoa amri ya kutotoka nje kwa mamilioni ya watu kwa nia ya kupunguza madhara hayo kwao kwa muda wa siku tatu tangu jana jumapili na hali hiyo inatarajiwa kuendelea hadi siku ya Jumatano.