Posts

Showing posts from August, 2015

ELEWA UNDANI WA UGONJWA WA KIFUA KIKUU (TB)-2

Image
Naendelea kuelezea undani wa ugonjwa wa kifua kikuu ambapo leo nitazitaja dalili zake. Dalili za kifua kikuu hutegemea sana ni mahali gani bakteria wa TB wanakuaw. Kwa kawaida bakteria wa kifua kikuu wanakuwa kwenye mapafu na kusababisha kifua kikuu cha mapafu.  Kifua kikuu cha mapafu kinaweza kusababisha kifua kikali kinachochukua zaidi ya wiki tatu, maumivu ya kifuani na kukohoa damu au makohozi. Dalili nyingine za ugonjwa wa TB ni pamoja na udhaifu au uchovu, kupungua uzito, kukosa hamu ya kula, baridi, homa na kutoka jasho usiku. Kifua kikuu tuli hakina dalili. TIBA  Kwa kawaida, mgonjwa wa kifua kikuu anatumia vidonge kila siku wakati wa matibabu yanayosimamiwa. Ugonjwa wa kifua kikuu kikali unaweza kutibiwa kwa mchanganyiko wa antibiotics. Mchanganyiko sahihi wa dawa za kifua kikuu hutoa kinga na tiba. Tiba inayofaa humwezesha haraka mgonjwa wa kifua kikuu kutoambukiza na kwa hiyo huzuia kuenea zaidi kwa kifua kikuu. Kufanikisha tiba ya TB, huchu

VIDEO: Haya Hapa MAKUBWA Yote Kutoka Kwa Mwanamke Pekee Anayetaka Kuwa Rais wa Tanzania 2015.

Image
Kampeni za uchaguzi mkuu wa Tanzania 2015 zimeshaanza tayari na tumewaona Wanasiasa mbalimbali wakisimama mbele ya Watanzania kutumia time yao kuwashawishi wapate zile YES za kutosha na hatimaye kuchukua nafasi ya uongozi na kuleta mabadiliko waliyoahidi. Miongoni mwa waliosimama mbele ya Watanzania kuzitaka kura za Urais ni pamoja na mgombea Urais kupitia chama cha ACT WAZALENDO Anna Mghwira ambaye unaweza kuyapata yote makubwa anayoyasema kwa kutazama hii video hapa chini.

VIDEO Yenye Maneno MAZITO MANNE ya Zitto KABWE

Image
Kiongozi wa chama kipya cha kisiasa Tanzania ACT WAZALENDO Zitto Kabwe alikua miongoni mwa waliosimama kuzungumza kwenye siku ya kwanza ya kampeni za chama hicho Mbagala Dar es salaam ambapo mgombea Urais wao mwaka huu ni Mama Anna Mghwira. Kwenye hii video hapa chini utakutana na yote makubwa kutoka kwa Zitto Kabwe.

IMEKULA KWAKE! Sababu ya kushindwa kusajiliwa De Gea Real Madrid na maamuzi ya klabu hiyo kwa FIFA viko hapa…

Image
Golikipa wa kimataifa wa  Hispania  ambaye anaichezea klabu ya  Manchester United David De Gea,  alikuwa akihusishwa kujiunga na klabu ya  Real Madrid ya  Hispania,  hivyo kila kitu kilikuwa kimesha kuwa sawa ikiwemo maslahi binafsi ya mchezaji. De Gea  ambaye aliripotiwa usiku wa August 31 kuwa karibu na kujiunga na  Real Madrid  timu aliyokuwa akihusishwa kujiunga nayo tokea zamani, mpango wa  De Gea  kujiunga na timu hiyo ulikwama baada ya viongozi wa  Man United kuchelewa kutuma mikataba katika klabu ya  Real Madrid,  hivyo walituma dakika moja baada ya dirisha la usajili kufungwa. Tatizo la kuchelewa kwa  documents  za mikataba hiyo ni mfumo wa usajili wa FIFA  ndio umefanya  documents   kutoka klabu ya  Man United  kuchelewa kufika kwa  Real Madrid , kutokana na  Real Madrid  kuwa na ushaidi wa hizo  documents watakata rufaa  FIFA  ili wapewe nafasi ya kumsajili  De Gea  nje ya muda wa usajili kwani mfumo wa  FIFA  ndio uliochelewesha usajili huo. Klabu ya  Real

Mtoto wa mchezaji bora wa dunia kutokea Brazil amejiunga na klabu hii ya Ulaya!

Image
Mtoto wa mchezaji wa zamani wa  FC Barcelona  na timu ya taifa ya  Brazil Rivaldinho Rivaldo  ambaye anafuata nyayo za baba yake  Rivaldo  katika soka, amesajiliwa na klabu ya  Boavista  ya  Ureno  akitokea klabu ya  Mogi Mirim  ya kwao  Brazil . Hivyo hiyo inakuwa mwanzo wa safari yake ya kusaka mafanikio kama aliyoyapata baba yake  Ulaya . Rivaldinho  ambaye ana umri wa miaka 20 amejiunga na klabu ya  Boavista  kwa mkataba wa miaka mitatu na kuhama katika klabu ambayo baba yake mzazi ni Rais, hiyo itamfanya kukua na kukomaa kisoka kwani ataanza kuishi mbali na uangalizi wa baba yake. Mchezaji huyo ambaye amepata umaarufu kutokana na ukubwa wa jina la baba yake, ni kawaida kuingia katika headlines kila mara anapofunga goli, ameichezea klabu ya  Mogi Mirim  jumla ya mechi 44 na kufunga goli 10.  Rivaldinho  ili aweze kufikia rekodi za baba yake inabidi ajitume kwani hadi sasa hajawahi cheza katika timu ya taifa ya  Brazil  hata ya vijana.

EPA: Watuhumiwa wa Sakata la EPA Washinda Kesi (Marando na Wenzake)

Image
Hukumu hiyo imesomwa jana. Upande wa mashitaka wameshindwa kuthibitishia mahakama juu ya makosa ya watuhumiwa! Taarifa kamili itawajia hapa hapa  http://winternews1.blogspot.com/  hivi punde!

VIDEO: Msichana Membo Akiiba Mbele za Watu Inakuaje? Jamaa Walitegesha Video Camera, Jionee Ilivyokua Hapa...

Image
Jamaa wametegesha video camera sehemu alafu wakatafuta Mwanamke mrembo ajifanye mwizi wa kuchomolea watu mfukoni, hii imetokea Marekani lakini najua kama wangetegesha hii camera kwenye nchi kama Tanzania mpaka watu wajue ni mchezo unachezwa tayari mtu ameshapokea kipigo. Nimekuwekea video hiyo hapo chini mdau! Waweza ipakua/download au play kuicheki!

VIDEO ya dakika 10 za LOWASSA mbele ya Wanawake wa Dar es salaam!

Image
Ilikua ni siku ambayo mgombea Urais 2015 kupitia ruhusa ya UKAWA Edward Lowassa alipokutana na Wanawake wa Dar es salaam siku kadhaa tu kabla ya uzinduzi wa kampeni za UKAWA 2015. Cheki/Download video hiyo hapo chini!

MATUSI mitandaoni Tanzania mwisho ilikua jana saa tano na dk 59 usiku ! Fahamu mengine ya sheria mpya hapa

Image
Huu ndio utakua mwisho wa makosa ya kimtandao Tanzania??? sababu sheria hii imepitishwa na kuanza kutumika leo mahususi kwa wote wanaotumia vibaya mtandao.   Unaambiwa mwisho wa yote ulikua jana August 31 2015 sababu leo September 1 2015 sheria hii ndio imeanza kutumika rasmi baada ya kupitishwa na Bunge mapema 2015 na kusainiwa na Rais Kikwete ikiwa ni miongoni mwa sheria zilizopitishwa na bunge kwa hati ya dharura.   Unafahamu sehemu ya makosa ambayo yanaweza kukufanya ushtakiwe ? Kuweka mtandaoni picha za kingono za watoto Kuweka mtandaoni picha za ngono au za utupu Kuweka taarifa za uongo mtandaoni Kuweka taarifa za uchochezi mtandaoni Kutukana au kumdhalilisha mtu Kuweka mtandaoni tetesi zisizothibitishwa Kutukana au kumdhalilisha mtu kwa misingi ya udini/ukabila.   Innocent Mungi kutoka Mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA) anasema >>>  ‘ Ambaye atakua anachukua maamuzi ni jeshi la Polisi ambaye kwa mfano mtu akitukana kwenye mtandao au kufanya chochote k

STAA Huyu Naye Aondoka Rasmi MANCHESTER UNITED

Image
Kocha Louis van Gaal ameendelea kusafisha timu kwa kuuza wachezaji au kuwatoa kwa mkopo. Baada ya mchana wa leo kumtoa kwa mkopo Januzaj, jioni hii klabu ya Manchester United imemuuza mshambuliaji wake Javier “Chicharito” Hernandez.    Mshambuliaji wa Mexico ameuzwa kwenda klabu ya Bayer Leverkusen na amesaini mkataba wa miaka 3 na klabu hiyo inayoshiriki ligi ya Ujerumani.    Chicharito aliyejiunga na United kutoka klabu ya  Guadalajara kwa ada ya £6.9m mwaka 2010, ameuzwa kwenda Leverkusen kwa ada isiyopungua kiasi cha £8.75 million

25 PHOTOS: Red carpet na Performance za wasanii kwenye MTV Video Music Awards (VMA’s)

Image
Tuzo za muziki za MTV VMA’s 2015 zilifanyika Jumapili, Agosti 30, Microsoft Theater, Los Angeles, Marekani. Hizi ni baadhi ya Picha za performance za wasanii waliotamba kwenye jukwaa pamoja na mastaa waliotokea poa kwenye red carpet ya tuzo hizo. Justin-Bieber Taylor Swi and Nicki-Minaj The-Weeknd Tori-Kelly2 Justin-Bieber Macklemore (center) performs on the Pepsi Stage, during the 2015 MTV Video Music Awards, at The Orpheum Theatre on August 30, 2015 in Los Angeles, California. Pharrell Williams performs on the Pepsi Stage, during the 2015 MTV Video Music Awards, at The Orpheum Theatre on August 30, 2015 in Los Angeles, California. artist Justin Bieber performs onstage during the 2015 MTV Video Music Awards at Microsoft Theater on August 30, 2015 in Los Angeles, California. Miguel. Kanye West na Kim Kadarshian Rita Ora. Miley Cyrus ambae alikuwa MC wa tuzo hizi Amber Rose n Blac Chyna walikuwepo pia Ciara John Legend na mke wake Kylie

MAGAZETI YOTE YA LEO JUMANNE TAREHE 1/9/2015...SIASA, UDAKU, MICHEZO NA BURUDANI!

Image
. . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .