CHAMA CHA ACT CHAWEKA HISTORIA, CHAVUNJA REKODI YA CHADEMA NA CUF



Akizungumzia historia iliyowekwa na chama hicho,Zitto alisema kuwa ACT kimeweza kusimamisha wagombea ubunge katika majimbo 219 kati ya majimbo 265 jambo ambalo linakifanya chama hicho kuwa ni chama cha pili kwa wagombea ubunge wengi huku cha kwanza kikiwa ni chama cha mapinduzi CCM.

Historia nyingine ambayo chama hicho kimeiweka ni kuweza kusimamisha wagombea ubunge wanawake wengi kuliko vyama vingine vyote nchini Tanzania ambapo chama hicho kimesimamisha wanawake 25% sawa na wabunge 55 katika majimbo toifauti tofauti nchini Tanzania huku kubwa ni kusimamisha mgombea urais mwanamke.

Zitto alitaja historia nyingine kuwa ACT wazalendo ndio chama pekee kilichosimamisha wagombea wenye umri mdogo kuliko vyama vyote nchini ambapo mgombea mwenye umri mdogo ana miaka 21 na mwingine akiwa na miaka 23 ambapo alisema kuwa ni ishara kuwa chama hicho kinawajali vijana.

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini