PENNY Agomea Arobaini ya TIFFAH

PENY
Mtangazaji Penniel Mungilwa ‘Penny’.
 Imelda Mtema
Mtangazaji Penniel Mungilwa ‘Penny’ ameibuka na kusema kuwa hata akialikwa kwenye sherehe ya arobaini ya mtoto wa ‘x’ wake, Nasibu Abdul ‘Diamond’, Tiffah hawezi kwenda pamoja na ushkaji wao kwa sababu mpenzi wake wa sasa hawezi kumruhusu.
 

Akizungumza na Ijumaa Penny alisema kuwa hawezi kwenda kwenye sherehe hiyo kwa sababu Diamond ni mtu ambaye alikuwa na uhusiano naye wa kimapenzi huko nyuma hivyo kwenda kwenye sherehe hiyo ni moja ya kumkwaza mpenzi wake wa sasa.
“Sina ubaya na Nasibu lakini siwezi kukanyaga kwenye sherehe ya mtoto wake kwa sababu siwezi kueleweka kwa baby wangu, kama mapenzi tulimaliza kitambo tutakutana tu kwa mambo mengine lakini siyo mimi kujibeba na kwenda kwake,” alisema Penny

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini