TAARIFA Muhimu Kwa Watumiaji wa WhatsApp

WhatsApp imeboresha zaidi huduma zake kwa kuongeza baadhi ya vitu ambavyo havikuwepo katika matoleo yaliyopita. Maboresho hayo ni kwa watumiaji simu za Android.
whatsapp-1
Katika version mpya 2.12.250, sasa mtumiaji wa WhatsApp anaweza ku-customize notifications kwa mtu mmoja mmoja au kwa kila kundi alilonalo, ikiwemo vibration length, popup notification, notification light na call notification tone.
Whatsapp2
Kingine anaweza kusoma ujumbe na kuurudisha uonekane haujasomwa au umesomwa kwa kubonyeza kwa muda mrefu bila kuachia chati husika.
Whatsapp3
Katika version mpya pia zimeongezwa ‘emoji’ mpya ikiwemo ya ‘kidole cha kati’.
Update hiyo sasa inapatikana kwenye Google Play Store.

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini