Posts

Showing posts from April, 2015

DIAMOND: BORA NIFE KULIKO KUMRUDIA WEMA

Image
Musa mateja KIAPO! Kuonesha kwamba hana mpango wa kurudi nyuma, staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platinumz’ amefungukia msimamo wake juu ya mwandani wake wa zamani, Wema Sepetu ‘Madam’ kwa kusema kuwa kamwe hawezi kumrudia tena, Risasi Jumamosi lina mkanda kamili. Staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platinumz’. Licha ya Diamond kufunguka hayo, wawili hao wamekuwa na mapenzi ya vipindi, kuna wakati waliwahi kumwagana kisha kurudiana na hakuna aliyewahi kutoa tamko zito lakini safari hii Diamond amesema ndiyo basi tena! TUJIUNGE NA CHANZO Kwa mujibu wa chanzo makini kilicho karibu na staa huyo, mara kwa mara Diamond amekuwa akijiwekea nadhiri ndani ya moyo wake na kusisitiza kwamba pamoja na kuwa maisha ya sasa huendeshwa kwa msingi wa fedha lakini hata kama ‘atafulia’ kiasi gani, ni bora afe maskini kuliko kurudiana na Wema. “Diamond amekuwa akisema kila wakati kwa msisitizo kuwa kutokana na matatizo aliyokumbana nayo katika uhusiano wake kwa

BASI, LORI VYAGONGANA USO KWA USO NA KUUNGUA MOTO

Image
WATU kadhaa wanahofiwa kupoteza maisha baada ya basi la Nganga la kutoka Dar kwenda Mbeya kugongana uso kwa uso na lori aina ya Fuso maeneo ya Mlimani kilometa kadhaa kutoka Ruaha-Mbuyuni, katika barabara ya Iringa-Morogoro ambapo magari yote mawili yameteketea kwa moto. Habari kutoka eneo la tukio zinasema kwamba mmoja wa watu waliofariki ni dereva wa Fuso.

MAUAJI YA KUTISHA MWIKA KILIMANJARO, WATUHUMIWA WA WIZI WACHOMWA MOTO HADI KUFA, PICHA 7 ZIKO HAPA

Image
 Polisi wakichukua mabaki ya miili ya marehemu hao baada ya kuchomwa moto.  Wakiteketea kwa moto  Watuhumiwa hao wakiwa hoi kwa kipigo kabla ya kuchomwa moto hadi kufa.  Wakiendelea kupokea kichapo kutoka kwa wananchi. Wananchi walioamua kujichukulia sheria mkononi, wamewaua watu wawili wanaodhaniwa kuwa ni wezi kwa kuwachoma moto mpaka kufa huko Mwika wilaya ya Moshi vijijini Mkoani Kilimanjaro Tukio hilo limetokea jana majira ya saa 6 mchana ambapo pia wameichoma moto pikipiki waliyokuwa wakiitumia watuhumiwa hao (ambao wamechomwa moto hadi kufa) Kwa mujibu wa taarifa za awali kutoka eneo la tukio bado hakuna mtu anayeshikiliwa kwa kuhusika na mauaji hayo

Rais Kikwete Apokea Ripoti Ya Oparesheni Tokomeza

Image
Rais Jakaya Kikwete jana alipokea Ripoti ya Uchunguzi wa Operesheni Tokomeza katika hafla fupi ilifanyika Ikulu, Dar es Salaam.   Mara baada ya kupokea ripoti hiyo, Rais Kikwete aliishukuru Tume kwa kazi nzuri na kuongeza kuwa amefurahi kuwa suala zima la Operesheni Tokomeza sasa limefika mwisho wake.   Aidha, Rais amesema kuwa Serikali itaisoma ripoti hiyo na katika wiki mbili itatoa maelezo ya jinsi ripoti hiyo itakavyoshughulikiwa.   Rais Kikwete amepokea ripoti hiyo kutoka kwa Jaji mstaafu Hamisi Msumi, Mwenyekiti wa Tume ambayo Rais Kikwete aliiteua Mei Mosi, mwaka jana, na kuitaka ichunguze tuhuma mbali mbali za uvunjifu wa Sheria, Kanuni, Taratibu na Hadidu za Rejea za Utekelezaji wa Operesheni Tokomeza.    Aidha, Rais Kikwete aliipa Tume hiyo jukumu la kupendekeza hatua stahiki za kisheria za kuchukua dhidi ya watakaobainika kuhusika na uvunjifu huo. Vile vile, Rais aliiagiza Tume hiyo ishauri namna bora ya utekelezaji wa operesheni kama hi

Ajali ya Lori na Pawatila Yaua Watu 7 Manyara

Image
Watu saba wamekufa na wengine saba kujeruhiwa katika ajali ya gari iliyotokea katika kijiji cha Endagau tarafa ya Endasaki wilayani Hanang’ mkoani Manyara baada ya lori aina ya Fuso kugongana na powatila.   Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, Christopher Fuime alisema lori hilo yenye namba za usajili T 781 AAC likitokea Katesh kuelekea Babati liligongana na pawatila iliyokuwa imebeba wakulima waliokuwa wakitokea shambani kuvuna maharage katika kijiji cha Getasam.   Kamanda Fuime alisema kwamba chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi wa fuso ambapo lilisababisha kupasuka kwa gurudumu la mbele ndipo lilipoteza mwelekeo na kuligonga pawatila na kusababisha watu sita kufa papo hapo na mmoja kupoteza maisha katika Hospitali ya Dareda wakati akipatiwa matibabu.   Aliwataja waliokufa ni Uttu (18) Mkazi wa Endasaki, Lazaro Daniel (30) mkazi wa Kijiji cha Maraa, Agustino Marcel (30) mkazi wa Kijiji cha Maraa, Inocent (16) Mkazi wa Maraa, Stephano Dahaye (18) Mkazi wa M

Taarifa ya Jeshi la Polisi Nchini Kufuatia Upotoshwaji Unaoenezwa Kwa Njia ya Mtandao ili Kuwatia Watu Hofu

Image
Katika siku za hivi karibuni kumeibuka tabia ya baadhi ya watu wachache wasiofahamika kutunga na kusambaza ujumbe kupitia simu za mikononi na mitandao mbalimbali ya kijamii wenye lengo la kuwatia hofu wananchi, jambo ambalo ni kinyume cha sheria. Aidha, watu hao wanaosambaza taarifa hizo wanajifanya kwamba taarifa hizo zimetoka kwenye taasisi za kimataifa na taasisi zingine zinazoaminika jambo ambalo siyo kweli. Jeshi la Polisi nchini linawataka wote wenye tabia hiyo kuacha mara moja na badala yake, endapo mtu yeyote anayo taarifa ya uhalifu wa aina yoyote ama kikundi chochote cha uhalifu atoe taarifa hiyo katika kituo chochote cha Polisi au kupitia simu za makamanda wa polisi wa mikoa ama vyombo vingine vya ulinzi na usalama ili taarifa hizo ziweze kufanyiwa kazi haraka. Aidha, Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi wa taarifa zote zinazopokelewa ili kuhakikisha kwamba usalama wa raia na mali zao unaendelea kuimarika.  Hata hivyo, Jeshi la Polisi halitasita

Baba Ahukumiwa Kifungo cha Maisha Jela Kwa Kosa la Kumbaka Mtoto wake Wa Miaka 9 na Kumpa Ujauzito

Image
Mahakama ya Hakimu Mkazi wilaya ya Shinyanga imemhukumu kifungo cha maisha jela mkazi wa mtaa wa Kitangili katika manispaa ya Shinyanga baada ya kupatikana na hatia ya kumbaka na kumpa ujauzito mtoto wake wa kambo, mwanafunzi wa darasa la tatu.   Alimbaka mtoto huyo kutimiza masharti ya mganga ili kutoa tiba kwa mkewe.   Akisoma hukumu hiyo jana, Hakimu Mkazi mwandamizi wa wilaya, Thomson Mtani alisema mahakama imeridhika na ushahidi uliotolewa na upande wa mashitaka ukiongozwa na wakili wa serikali, Judith Tuka.   Mtuhumiwa Osward Charles (45) mkazi wa Kitangili alifikishwa mahakamani kwa tuhuma mbili. Kosa la kwanza likiwa ni kumbaka mtoto wake mwenye umri chini ya miaka kumi ambaye ni mwanafunzi kinyume na kifungu namba 130, kifungu kidogo cha kwanza na cha pili na kifungu namba 131 kifungu kidogo cha pili cha sura ya 16 cha kanuni ya adhabu.   Kosa la pili ni kumwingilia kimwili mtoto wake ambaye ni mwanafunzi wa shule na kumpa ujauzito kinyume na k

LORI LAFELI BREKI NA KWENDA KUPARAMIA PRADO

Image
Lori la Mizigo lenye namba za usajili T 255 CRN na lililokuwa na Tela lenye namba za usajili T 478 BCG likiwa limefunga njia baada ya kufeli breki lilipo kuwa kwenye njia kubwa katika eneo la Mbezi Mwisho, Jijini Dae Es Salaam 

INATISHA SANA! MWANAJESHI AUA MKEWE KWA SHOKA, NAYE AJIUA HUKO MWANZA!

Image
Picha na maktaba ila siyo ya tukio hilo! Mashaka baltazar, Mwanza   ASKARI  wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Jacob Mponeja wa kikosi  cha 512  MCT Nyegezi, Mwanza, anadaiwa kumuua mkewe kwa kumkata na shoka kichwani kisha mwenyewe kujinyonga hadi kufa chumbani kwake, tukio lililotokea mwanzoni mwa wiki hii jijini Mwanza.   Habari kutoka kwa watoto wa marehemu zinasema, kabla ya tukio hilo, wanandoa hao walikuwa na ugomvi unaodaiwa ulitokana na wivu wa kimapenzi. Mmoja wa watoto wa marehemu, Sara Mponeja, akizungumza na waandishi wa habari, alisema marehemu  mama yake awali alikuwa safarini Bariadi mkoani Simiyu, ambapo alirejea nyumbani  Ijumaa wiki iliyopita.   Alisema baada ya kurejea, alikuta ujumbe mfupi wa maneno ‘sms’ katika simu ya baba yao ndipo ugomvi baina yao ulipoanza.“Hali hiyo iliendelea na juzi usiku baada ya chakula kuandaliwa, baba aligoma kula, ndipo mama naye alikataa kula. Wakati tumelala, tulisikia kelele za ugomvi, ingawa mwanzoni tulichuku

TUKIO LA KIGAIDI KENYA MTUHUMIWA AKAMATWA

Image
Said Swaleh Said Awadh. He was arrested by the Anti-Terrorism Police Unit (ATPU) officers in Mandera on Monday March 30, 2015. He is suspected to be involved in the killing of moderate Muslim clerics at the Coast.  PHOTO | FRED MUKINDA | NATION MEDIA GROUP Police arrest man suspected to be behind killing of moderate Muslim clerics. Police have arrested a man in connection with the killing of moderate Muslim clerics at the  Said Swaleh Said Awadh was arrested by the Anti-Terrorism Police Unit (ATPU) officers in Mandera on Monday. Security sources told the Nation that the man was on his way to join Al-Shabaab in Somalia. He was interrogated over the killing of Sheikh Mohamed Idris. Sheikh Idris was the chairman of the Council of Imams and Preachers of Kenya before he was killed in June 2014. Sheikh Idris was felled after gunmen opened fire close to a mosque near his home. Before his death, he was at the forefront in the fight against radicalisation of the youth at the Coas

Rais Kikwete Aombwa Kutoupitisha Muswada wa Sheria ya Makosa ya Mtandaoni, 2015 ....Ombi Hili Limetolewa Na Chama cha Bloggers Tanzania (TBN)

Image
Mtandao wa waandishi kupitia mitandao nchini, Tanzania Bloggers Network (TBN) tunamuomba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete kutumia mamlaka yake vyema kwa kutokupitisha muswada wa Sheria ya Makosa ya Mtandao, 2015 unaokandamiza uhuru wa mawasiliano mitandaoni.     Muswada wa sheria ya makosa ya Mtandaoni unaainisha makosa yanayohusiana na matumizi ya mfumo wa kompyuta na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, na kuweka utaratibu wa upelelezi, ukusanyaji na matumizi ya ushahidi wa kieletroniki na masuala mengine yanayohusiana na hayo.   Muswada  Wa  Sheria  Ya  Makosa  Ya  Mtandaoni,2015 Umoja huu (TBN) ulishtushwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kukubali kupitisha Muswada wa Sheria ya Makosa ya Mtandao 2015 kwa hati ya dharura kitendo ambacho hakikutarajiwa kutokana na kuwa mitandao bado ni kitu kipya nchini hivyo tulihitaji maridhiano na wadau na elimu kati ya raia na Serikali ili wengi watambue yapi ni makosa kwa ku

Taarifa kuhusu upotoshaji wa mswada wa Sheria ya Makosa ya Mtandao 2015

Image
  Taarifa kwa vyombo vya Habari , 4 Aprili 2015 Taarifa kuhusu upotoshaji wa mswada wa Sheria ya  Makosa ya Mtandao 2015 Naomba nifafanue kuhusu propaganda inayoenezwa na maafisa wa TCRA kupitia CloundsFM kuhusu Sikika na Mswada wa ‪#‎CyberCrimeBill‬. Sikika haikuhudhuria mkutano wa wadau unaodaiwa kufanyika Dodoma kama ilivyodaiwa na Mh Peter Serukamba na leo maafisa wa TCRA. Sikika haikutoa maoni kuhusu Mswada wa miamala ya kielektoniki kama ilivyodaiwa na Mh Peter Serukamba na pia leo maafisa wa TCRA. Sikika ilituma maoni ya pamoja ya wadau kwa niaba ya wadau kuhusu #CyberCrimeBill kwa njia ya email kwa Mkiti Kamati Mh Peter Serukamba. Maoni hayo hayakutumika kuboresha #CyberCrimeBill bali kuongeza tu orodha ya wadau wanaoda iwa "kushiriki" kwa lengo la kuonesha kuridhia. Kwa kuwa maoni ya wadau hayakuzingatiwa na kwamba ‪#‎CiberCrimeBill‬ iliyopitishwa ina mapungufu mengi, Sikika na wadau bado wanaipinga. Mwisho tunaomba

Picha:Reginald Mengi amefunga ndoa na Jacqueline Ntuyabaliwe

Image
Hizi  ni  Picha  kutoka kwenye harusi  Reginald  Mengi ambayo imefungwa kwenye ardhi ya nchi ya Mauritius  mwisho wa mwezi March 2015.    Hii ndoa pia ilishuhudiwa na watoto wao wawili mapacha kama wanavyoonekana kwenye picha pamoja na marafiki wengine wa familia pamoja na ndugu ambao idadi yao inafikia 50.   Ndoa imefungwa miezi minne baada ya Reginald Mengi kumchumbia Jacky Dubai kwenye siku ya kuzaliwa ya mrembo huyu December 2014.             Picha  kwa  hisani  ya  Bongo5

Kardinali Pengo Asali Chini ya Ulinzi Mkali.....FFU Wakiwa Na Mbwa 8 Waliweka Doria Kuimarisha Ulinzi

Image
Katika  hali isiyo ya kawaida, Polisi wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) wakiwa na mbwa nane, waliweka doria katika Kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es Salaam wakati wa ibada ya Ijumaa Kuu iliyofanyika jana.   Ibada hiyo iliyoanza saa tisa jioni iliongozwa na Paroko wa Kanisa hilo, Audax Kaasa na Mwadhama Kardinali Polycarp Pengo aliyetarajiwa kuiendesha kama ratiba ya Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) ilivyoeleza, lakini hakufanya hivyo bali alisali kama muumini wa kawaida.    Gari ya polisi yenye namba PT 0964 iliegeshwa karibu na lango kuu la kuingilia kanisani humo, huku mbwa kadhaa wakizunguka katika maeneo mengine kuangalia usalama na baadaye waliingizwa katika gari hilo.   Haikujulikana sababu ya ulinzi huo katika kanisa hilo kwa kuwa makanisa mengine makubwa likiwemo Azania Front hakukuwa na hali hiyo.   Baadhi ya wadadisi wa mambo wanaihusisha hali hiyo na sakata linaloondelea kati ya Pengo na Kiongozi wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Askof

Hakimu wa kesi ya mauaji ya Dk. Mvungi ajitoa

Image
Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Waliarwande Lema, amejitoa kusikiliza kesi ya mauaji ya kukusudia ya aliyekuwa mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Dk. Sengondo Mvungi, inayowakabili washtakiwa 11.   Tukio hilo lilitokea juzi, baada ya washtakiwa hao 11 kumuomba Hakimu Lema ajitoe kuisikiliza kesi yao ili iweze kupangwa kwa hakimu mwingine ambaye wao wanaona atawatendea haki.   Kutokana na ombi hilo, Hakimu Lema alijitoa na kuiahirisha kesi hiyo ambayo upelelezi wake hadi sasa bado haujakamilika na itatajwa tena AprilI 20, 2015, itakapopangwa mbele ya Hakimu mwingine.   Mawakili wa Serikali, Ofmad Mtenga na Diana Lukondo walidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na waliomba ipangiwe tarehe nyingine kwa ajili ya kuitaja.   Miongoni mwa washtakiwa wanaokabiliwa na kesi hiyo ni Chibago Magozi (32), John Mayunga (56), Juma Kangungu (29), Paulo Mdonondo (30), Mianda Mlewa (40), Zacharia Msese (33), Msungwa Matonya (30), Ahm