Jeshi la polisi jijini Tanga lasambaza askari wake kuimarisha ulinzi katika kipindi hiki cha sikukuu

Jeshi la polisi mkoani Tanga limesambaza askari katika makanisa yote jijini Tanga kufuatia hivi karibuni kuibuka kwa viashiria vya ugaidi vilivyosababisha waumini wa madhehebu mbali mbali kuwa na hofu kwenda katika mkesha wa sikukuu ya pasaka.

Akizunguza jijini Tanga kuhusu jitihada za jeshi katika kuimarisha ulinzi na usalama katika nyumba za ibada kuanzia jana kwenye ibada za ijumaa kuu hadi jumatatu ya pasaka,kaimu kamanda wa polisi mkoani tanga Bwana Juma Ndaki amewataka waumini wasiwe na hofu hata kama wakiona idadi kubwa ya askari katika nyumba za ibada kwa sababu ni sehemu ya utekelezaji katika zoezi la kuimarisha ulinzi na usalama.
 
Katika hatua nyingine mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Daleda Masaka amekufa baada kuanguka katika mapango ya amboni wakati alipokuwa akivunja mawe kwa ajili ya kupata kokoto ndipo alipokanyaga jiwe kubwa lililokuwa limejiegesha katika shimo ambalo hutumika kuweka baruti kwa ajili ya kulipua mawe kisha kutumbukia na kufunikwa na jiwe hilo.
 
Kufuatia hatua hiyo mratibu wa makundi yanayojihusiha na kuponda mawe kwa ajili ya kutengeneza kokoto amewaagiza wadau wa kazi za kuvunja mawe kuacha zoezi hilo mara moja kufuatia mvua zinazoendelea kunyeesha kuharibu sehemu ya mawe na kusababisha kuteleza na kuanguka kutoka milimani hatua ambayo inaweza kusababisha madhara makubwa zaidi ya hayo.

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini