Posts

Showing posts from May, 2015

NJIA SABA (7) ZA UHAKIKA ZA KUPATA AJIRA HIZI HAPA

Image
pay per click advertising Kupata nafasi za ajira imekuwa ngumu siku hadi siku, hususani ukitilia maanani kuwa wahitimu wanazidi kuwa wengi na hali ngumu ya uchumi inafanya waajiri kushindwa kuongeza nafasi mpya za kazi. Hauna haja ya kukata tamaa ya kupata kazi ile unayoitarajia hata kama kuna ukiritimba mwingi katika soko la ajira kama vile watu kupeana kazi kwa kujuana, nafasi za kazi kutotangazwa   au kazi haipatikani mpaka rushwa itembee. Makala hii inaenda kujadili mambo ya msingi kwa yeyote anayetafuta kazi, uwe kwa sasa umeajiriwa unatafuta kazi mbadala au uwe hauna ajira unatafuta ajira, bila shaka mambo tunayojadili hapa yatakusaidia. 1.Mtazamo wako kuhusu ajira: Fahamu kuwa  bidhaa  ni chochote kile ambacho kinatimiza mahitaji fulani. Mwenye kuhitaji bidhaa huwa tunamuita  mteja .    Muajiri anatafuta mfanyakazi kwa kuwa analo hitaji la kazi fulani kukamilika, na anayo matarajio kadhaa toka kwa mfanyakazi anayemuajiri.     Hivyo wewe kama mfanyakazi mta

HABARI HII FEKI IMEWAHADAA WENGI FACEBOOK

Image
pay per click advertising pay per click advertising Hivi karibuni katika mtandao wa FACEBOOK kumezagaa post inayoeleza uwepo wa VIDEO inayoonyesha NYOKA AKIMLA MAMBA. Na ukibofya link husika utaaambiwa kwanza SHARE hiyo habari ili uweze kufungua hiyo video. Na hata uki share hakuna KITU cha ziada. Huo ni UZUSHI tuu. Kuna watu wanaamua kucheza na AKILI ZAKO ili kukudharirisha kwa kuonyesha kuwa haupo makini. Ipo hivi:- -- Wewe mwenyewe kabla ya ku share jiulize kama kweli video ipo kwa nini wasiruhusu tuu ionyeshwe mpaka eti wewe ufanye KUSHARE hiyo habari. ---Je, haukuweza ku hakiki taarifa hii kwa kusearch kwa GOOGLE kwa mfano ? ---Kwa nini ukubali kulazimishwa ku SHARE taarifa? Kuwa makini na taarifa za uongo wa namna hii , wajanja wanaweza kutumia kuingia kwa akaunti yako wakaiba taarifa zako au hata kuamua kupost kwa wall yako kwa niaba yako. Cheki picha ya post ninayoizungumzia hapa chini kwenye comment. pay per click advertising Niliandika kuhusu hab

Hawa walisherekea kifo cha Mwalimu Nyerere, leo wanamtumia kuutaka urais!

Image
pay per click advertising Tuachane na Josephat Gwajima anayejiita ni mchungaji japo sijui nani alimtunuku uchungaji na kwavigezo vipi, yeye hana tofauti na sigara kali Aliyekuwa anaamini Kingunge ni kiongozi wa kitaifa atafakari upya,Jiulizeni kwa nini hakupata nafasi ya juu kama Mzee Kawawa enzi ya mwalimu? Ni Kingunge huyuhuyu alifukuzwa ukuu wa mkoa singida na Mwalimu Nyerere, leo anajivika chanda cha Mwalimu. Lowa alifukuzwa uanachama wa TANU kwakosa la kuiba pesa ya ujenzi wa ofisi za umoja wa vijana wa Tanu jijini Arusha yeye akiwa ni katibu wa vijana mkoa, Ni Moringe na baadhi ya wazee waliopiga magoti kumuombea punguzo la adhabu na hivyo akapewa adhabu ya kuwepo Lumumba tu bila kazi yoyote kwa mda wa mwaka mzima. Katibu wa vijana TANU Taifa ndugu Elly Anangisye alifukuzwa moja kwa moja na ubunge wa Rungwe akavuliwa. Alipofariki tu Mzee Nyeree, Lowasa na kundi lake walifanya party na kupongezana, wengine walipigiana simu hata kabla hajafa kuwa kikwazo

Mwigulu Nchemba Kutangaza Nia ya Kugommbea Urais Leo Saa 9 Alasiri Chuo cha Mipango, Dodoma

Image
pay per click advertising Mwigulu  Nchemba  Kutangaza  Nia  ya  Kugommbea  Urais  Leo  Saa  9  Alasiri. Kama  kawaida, Mpekuzi  itakuwa  hewani  kukupatia  dondoo  muhimu za  sera  yake. Itarushwa Live na Star TV

Lucy Komba: Shida Kuubwa Tuliyonayo Wasanii...'Ukiwa na Kijana Utaambiwa Hufanani Nae Ukiwa na Mbabu Utaambiwa wa Nini'

Image
</script> SHIDA KUUBWA TULIYONAYO WASANII ukiwa na mwanaume kijana utaambiwa hufanani nae, ukiwa na mbabu utaambiwa vijana wote waliojaa mjini mbabu wa nini, ukiwa na kijana ambaye hana hela utaambiwa na umaarufu wote huo umekosa mwanaume mwenye hela, ukiwa na tajiri utasikia anasura mbaya lakini pesa sabuni ya roho, ukiwa na mzungu mzee utaambiwa huna lolote usubiri madakesi tu, ukiwa na mzungu kijana utaambiwa mzungu gani hana hela. Sasa je tufanyaje? Tuchagulieni nyie basi wa kufanana na sie. Lakini mimi naangalia moyo wangu unavyoniambia siangalii ya binadamu hasa sisi weusi maneno hayakauki. By Lucy Komba on Instagram pay per click advertising

Sentensi 18 za Edward Lowassa akitangaza kugombea Urais Arusha

Image
pay per click advertising May 30 2015 inakuwa siku ambayo inaingia kwenye Historia kubwa kwenye ishu za siasa Tanzania.. bado miezi michache ufanyike uchaguzi mkuu, mmoja ya watu ambao walitajwa sana na kuwa kwenye headlines kubwa kwenye vyombo  vya habari ni Mbunge wa Monduli, Edward Ngoyai Lowassa. Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Amri Abeid katikati ya Jiji la Arusha ulishuhudia kwa mara nyingine kujaa kwa watu ambao walikuja kushuhudia Mbunge huyo akitangaza nia ya kugombea Urais mwaka huu. “Watanzania wanahitaji mabadiliko, nina uwezo wa kusimamia mabadiliko hayo.. Mwalimu Nyerere alisema Watanzania wasipoyapata mabadiliko hayo ndani ya CCM watayatafuta nje ya CCM. sina shaka tukijipanga vizuri ndani ya CCM tunaweza kuwapa Watanzania mabadiliko wanayoyataka”   Edward Lowassa. “Nchi yetu inahitaji viongozi wenye sifa hizi.. uongozi wenye uthubutu usioogopa kufanya maamuzi magumu, uongozi usioyumba.. aweze kuwaunganisha Watanzania na kutoa utofauti kati ya walionacho n

Baada ya Jana Lowassa Kutangaza nia Urais 2015..January Makamba Nae Aja na Mpya...

Image
pay per click advertising Tume ya taifa ya uchaguzi imeshatangaza kwamba uchaguzi mkuu utafanyika October 2015 ambapo sasa ni headlines zake zinachukua nafasi kwa watu mbalimbali kutangaza nia za kugombea nafasi ya juu ya Urais. Post hii inamilikiwa na January Makamba ambae ni Mbunge wa Bumbuli Tanga na anautaka Urais pia ambapo May 30 2015 aliandika : pay per click advertising  ‘ Wiki ijayo tutataarifu ni lini na kwa namna gani tutazungumza na Watanzania, kuchukua fomu, kuanza safari za mikoani kukutana na Watanzania ‘ pay per click advertising

AJABU:Mwanaume Apandikiziwa Uso wa Mtu Mwingine Baada ya Uso wake Kuaribika na Kuwekewa Sura ya Mtu aliyekufa

Image
Picha ikimwonyesha Norris kabla hajapata ajali, alivyopata ajali na baada ya kuwekewa uso mwingine wa marehemu pay per click advertising Ajali nyingi duniani zimekua zikisababisha vifo vya watu wengi huku zikiacha wengine wakiwa na ulemavu wa maisha ambao huwasababishia kupoteza mwelekeo wa maisha yao na kukata tamaa kabisa. Pamoja na wengi kubaki na ulemavu, lakini pia madaktari wamekuwa kijitahidi kadri wawezavyo kuwarudisha watu hao katika hali zao lakini moja ya tukio la kushangaza ni la kijana Richard Norris ambaye alipata ajali mbaya na kumpelekea kuharibika vibaya sura yake. pay per click advertising Unaambiwa baada ya ajali hiyo kijana huyo alishindwa kutoka nyumbani kwa takribani miaka 15 na amini usiamini kijana huyo alifanyiwa upasuaji wa kihistoria uliochukua masaa 36 na kupandikizwa uso mpya wa mtu ambaye alishafariki baada ya kupata ajali. Upasuaji huo ulifanyika katika hospitali ya University of Maryland Medical Center na ulifanikiwa kwa kiasi kiku

Dudu Baya kurudi rasmi kwenye muziki kwa jina jipya, ‘Dudu Mamba’

Image
pay per click advertising Msanii wa Hip Hop wa muda mrefu, Godfrey Tumaini aka Dudu Baya amedai kujipanga kurejea rasmi kwenye muziki wa Hip Hop na kuahidi kuweka ushindani mkubwa na wasanii wenzake wakiwemo Fid Q na Young Killer Msodoki. Dudu Baya ameimbia Bongo5 kuwa si kwamba anarudi na muziki mpya tu bali pia akiwa na jina jipya – Dudu Mamba. “Ushindani nitauweza najua kuna wasanii kama Fid Q, Young Killer na wengine wanafanya vizuri lakini mimi sasa hivi nimekuja kushindana,” amesema Dudu Mamba. “Unajua hii miaka miwili nilionekana kutokuwa serious na muziki lakini sasa hivi tayari nimeshaingia studio za Mona Gangster. Mona ndo kamtoa Young Killer ngoma zote na wasanii wengine, kwahiyo tayari silaha ya kwanza katika kurudi kwangu ni kufanya kazi katika studio bora chini ya producer bora Mona Gangstar. Silaha ya pili ni mpangilio wa promotion ya ngoma yangu mpya. Nimeshazungumza na wadau mbalimbali wa media kuangalia jinsi gani tunawezafanya kazi kwa kushirikiana,

Afungwa miaka 30 kwa kumbaka mtoto wa miaka tisa

Image
pay per click advertising Mkazi wa Malampaka mkoani Simiyu, Benedictor Bulobo (30) , ametupwa gerezani atakakotumikia kifungo kwa miaka 30 baada ya kupatikana na hatia ya kumbaka binti wa miaka tisa.  Alihukumiwa  na Mahakama ya Wilaya ya Maswa juzi na Hakimu Mwandamizi Mfawidhi  Agatha Chigulu, baada ya kuridhishwa  na ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka. Akitoa hukumu hiyo hakimu huyo alisema kuwa anatoa adhabu hiyo ili kukomesha vitendo hivyo na kuwaonya wenye nia  mbaya ya kutaka kutenda kosa kama hilo wajifunze na kuacha mwenendo huo. Chigulu alieleza kuwa kosa hilo ni kinyume na kifungu cha 131 cha sheria ya kanuni ya adhabu sura ya 16 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2012. pay per click advertising  Awali mahakama iliambiwa na  Mwendesha Mashitaka wa Polisi, Nassibu Swedy kuwa mshitakiwa alitenda kosa hilo Februari 23 mwaka jana  saa 5:00 asubuhi. Alimnajisi mtoto huyo  maeneo ya nyumbani kwake baada ya kumkamata  kwa nguvu binti huyo mwanafunzi wa da

Majambazi wampora bunduki askari, Pwani

Image
IGP Ernesrt Mangu  Dar/Pwani. Matukio ya uporaji bunduki askari kwa watu wanaosadikiwa kuwa majambazi, yameanza kujipenyeza katika jiji la Dar es Salaam huku mkoa wa Pwani wakiendelea kuvamia na kuvunja vituo vya polisi. pay per click advertising Katika siku za karibuni, matukio hayo yametokea katika mikoa ya Pwani, Morogoro, Geita, Tanga na Mtwara ambako uporaji wa silaha ulitokea. Uporaji ulivyofanyika Watu 10 wanaosadikiwa ni majambazi wakiwa na mawe na mapanga wamemnyang’anya bunduki aina ya SMG na risasi 30, askari polisi wa Kituo cha Tazara kilichopo eneo la Yombo Station na kutokomea kusikojulikana. pay per click advertising Kamanda wa Polisi Kikosi cha Tazara Dar es Salaam, Patrick Byatao alisema Mei 27 mwaka huu saa 1:00 usiku, askari namba H.1574 PC Jineneko, alinyang’anywa SMG yenye namba 56-1402621 na risasi hizo huku majambazi hao wakimshambulia kwa mawe na mapanga. Byatao alisema kuwa, siku ya tukio askari D.8386 SGT Jum

Matapeli wavamia usajili wa wachezaji

Image
Mwenyekiti wa Kamati ya usajili ya Simba, Zacharia Hanspope  pay per click advertising Na Oliver Albert Dar es Salaam. Wakati usajili wa wachezaji nchini ukiendelea kushika kazi, kumezuka wimbi la watu wanaojifanya mawakala, wawakilishi wa wachezaji, kumbe ni matapeli, gazeti hili limebaini. Awali, mwenyekiti wa kamati ya usajili ya Simba, Zacharia Hanspoppe aliliambia gazeti hili kuwa matapeli hao wanaojifanya mawakala wamekuwa wakishiriki kupanga bei na hata mikataba ya wachezaji. Mawakala hao uchwara, Hanspoppe (pichani)amedai hawana leseni zinazotambuliwa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) au lile la Kimataifa (Fifa), wamekuwa wakiwapotosha baadhi ya wachezaji na kuwaingiza katika mizozo na klabu. pay per click advertising Alisema viongozi wa soka nchini hawana budi kuwa makini na mawakala wa wachezaji walioanza kujitokeza kipindi hiki cha usajili, wakipanga bei za wachezaji bila kufuata utaratibu. Aliongeza kuwa kipindi

Sitta atangaza nia ya urais ‘kiaina’

Image
pay per click advertising Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta  Dodoma/Dar. Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta amesema kati ya waliojitokeza na wanaotajwa kuwania urais, hakuna ambaye anaweza kupambana na kuikataa rushwa na kwamba muda ukifika ataweka hadharani nia yake. Sitta, ambaye pia anatajwa kuwania urais kwa tiketi ya CCM, alisema si ajabu na yeye kushawishika kujiunga na watangaza nia hao. pay per click advertising “Nikitazama hizi orodha zinazotajwa, sioni mtu anayepambana hasa na suala hili (la ufisadi). Nataka tuongeze nguvu ya wazalendo kupambana na ufisadi na tuwe wa vyama vyote,” alisema spika huyo wa Bunge la 10 Akizungumza na gazeti hili nje ya viwanja vya Bunge baada ya kuulizwa ni lini atatangaza nia ya kugombea urais, Sitta alisema: “Ni namna ya kuangalia mambo tu, bado kidogo maana muda upo mpaka Julai. Nyinyi (waandishi) subirini tu nitawaarifu.” Wasira, Mwigulu leo pay per click advertising Mchakamchaka wa kutangaza nia unaende

Lipumba: Vyombo vya dola vinashiriki ushirikina

Image
wenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba amesema baadhi ya watumishi wa vyombo vya dola wanashiriki au kuamini ushirikina na ndiyo maana wanaowafanyia ukatili watu wenye ulemavu wa ngozi (albino) hawakamatwi. pay per click advertising Akizungumza na wakazi wa mjini Tabora na Urambo katika ziara yake ya kuhamasisha wananchi kujiandikisha kwenye Daftari la Wapigakura, Profesa Lipumba alisema tatizo la kukatwa viungo au kuuawa kwa watu wenye ulemavu wa ngozi linatokana na baadhi ya watu katika vyombo hivyo vya dola kuhusika. pay per click advertising “Haiwezekani matukio yanatokea dhidi ya ndugu zetu na wahusika hawakamatwi, hii ina maana wapo wanaoamini katika ushirikina,” alisema. Profesa Lipumba aliwaambia wakazi hao kuwa miaka 54 baada ya uhuru, watu wenye ulemavu wa ngozi wanaishi kwa hofu kwa vile baadhi ya watu wanatafuta viungo vyao kwa lengo la kutafuta utajiri. pay per click advertising “Watu wenye ‘albinism’ wenyewe hawana uta

ARSENAL YATWAA KOMBE LA FA KWA KUICHAPA ASTON VILLA 4-0

Image
pay per click advertising pay per click advertising pay per click advertising Mabingwa mara 12 wa Kombe la FA, Arsenal baada ya ushindi wa leo dhidi ya Aston Villa. pay per click advertising Arsenal wakisherehekea ubingwa wao wa FA. pay per click advertising Theo Walcott akiifungia Arsenal bao la kwanza katika dakika ya 40. pay per click advertising Walcott akishangilia bao hilo. pay per click advertising Alexis Sanchez (kushoto) akipiga shuti lililojaa wavuni na kuiandikia Arsenal bao la pili. pay per click advertising Per Mertesacker akipiga mpira wa kichwa uliozaa bao la tatu kwa Arsenal. pay per click advertising Olivier Giroud akifanya hitimisho kwa kutupia kambani bao la nne. ARSENAL imetwaa Kombe la FA baada ya ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Aston Villa katika fainali iliyopigwa katika Uwanja wa Wembley usiku huu. Mabao ya ushindi ya Arsenal yamefungwa na Theo Walcott dakika ya 40, Alexis Sanchez daki

Aunty Ezekiel Responds To Her Haters Who Say Moze Iyobo Isn't The Daddy of Her Daughter Cookie

Image
pay per click advertising pay per click advertising Few days ago some of Aunty Ezekiel's friends  went to media to say that Aunty's daughter Cookie doesn't look like Moze Iyobo who is Aunty's boyfriend. Her friends whose names were withheld think the father of her daughter is someone else and not Moze Iyobo claiming the baby is white while both Moze and Aunty are black. But through instagram Aunty posted the photo above sharing hot kiss with Moze and insisted Moze is the daddy of her child... pay per click advertising pay per click advertising