Mwigizaji maarufu enzi za RTD, Bi Nyakomba aaga dunia



Bi Nyakomba ameaga dunia.

Marehemu Bi Nyakomba alipata umaarufu katika michezo ya maigizo redionio wakati huo ikirushwa na Redio Tanzania (RTD) akishirikiana na wasanii wenzake wakiwemo Hamisi Tajiri al maaruf Meneja, Ibrahim Raha al maaruf Mzee Jongo, Bakari Mbelemba al maaruf Mzee Jangala, Mzee Kagunga, Mzee Majengo na wengine, amefariki katika hospitali ya Jeshi la Polisi katika barabara ya Kilaw, alikopelekwa usiku wa kuamkia jana baada ya kuzidiwa.

Bi Nyakomba alikuwa akiugua kisukari tangu mwaka 2012.
Mwili wa marehemu Nyakomba unatarajiwa kuzikwa kesho saa tisa alasiri kwenye makaburi ya Chang'ombe jijini Dar es Salaam mara baada ya ibada ya mazishi itakayofanyika katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Maurus, Kurasini.

Ndugu wa familia ya marehemu wamesema Bi Nyakomba amefariki akiwa na umri wa miaka 64 akiacha watoto sita na wajukuu kumi na watatu.
Enzi za uhai wake, Channel TEN iliwahi kufika katika nyumba yake huko Keko Juu katika Kata ya Mburahati, Manispaa ya Temeke ili kumjulia hali wakati akiugua ambapo pamoja na mambo mengine, alihusia wasanii hususan vijana kote nchini, kuifanya sanaa kaw nidhamu kwa kuwa ni kazi rasmi kama nyinginezo.
Mwenyezi Mungu alitoa na ametwaa, jina lake lihimidiwe.
Apumzike pema marehemu Bi Nyakomba.
Pole kwa nyote mlioguswa na msiba huu.

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini