Nampenda sana Wema ila bado ana chuki na mimi – Kajala

 
 Kajala Masanja amesema hadhani kama ni rahisi kuwa karibu tena na Wema Sepetu baada ya kugombana.

Kajala amekiambia kipindi cha The Sporah Show hivi karibuni kuwa bado anampenda Wema na kumheshimu.

“Mimi simchukii Wema, mimi nampenda Wema, kusema ningependa kurudisha urafiki na Wema inakuwa ngumu sana, kwa sababu yeye tayari anachuki na sijui ana chuki kiasi gani? Mimi nataka kusema ni mtu ambaye nampenda na nakaaga nasema namheshimu, ni mtu ambaye alinisaidia,” alisema Kajala.

Pia Kajala amekanusha kutembea na mpenzi wa zamani wa rafiki yake huyo hali iliyozua ugomvi baina yao na kusababisha mpaka sasa kutoelewana.

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini