Posts

Showing posts from January, 2015

DIAMOND THE PLATNUMZ AWARUSHIA BURUNGUTU LA MAMILION MASHABIKI WAKE KWENYE TAMASHA LA TIGO KIBOKO YAO LEADERSCLUB

Image
 

MGOMO WA WAENDESHA DALADALA JIJINI MWANZA

Image
Daladala zikiwa zimepaki katika Jiji la Mwanza kutokana na mgomo wa madereva. Taswira kutoka maeneo ya Jiji la Mwanza baada ya mgomo wa waendesha daladala. WAENDESHA magari ya kusafirisha abiria katika ya Jiji la Mwanza maarufu kama daladala leo wamefanya mgomo na kuziba njia zote zinazoingia mjini kutokana na maeneo waliyokuwa wanaegesha magari yao kwa ajili ya kusubiri abiria (stendi) kugawiwa wafanyabiashara ndogondogo maarufu kwa jina la machinga kwa aijili ya shuhuli zao. Daladala zikiwa zimeegeshwa wakati wa mgomo. Hali hiyo imetokea leo asubuhi katika eneo la Stendi ya Tanganyika na Stend ya Soko Kuu jijini Mwanza ambapo yanaegesha magari ya kwenda Airport, Ilemela, Bwiru na Mwaloni ambapo madereva hao waliziba njia zote zinazo ingia kwenye maeneo hayo. Mwenyekiti wa waendesha daladala Mkoani Mwanza, Hassan Dede Petro alisema hali hiyo imejitokeza kutokana na wafanyabiashara hao kuanza kugawana maeneo kwenye stendi hizo bila uongozi wa waendesha daladala

MBUNIFU WA MAVAZI WA KIMATAIFA, SHERIA NGOWI AMVALISHA RAIS MPYA WA ZAMBIA

Image
Rais mpya wa Zambia, Edgar Lungu akiwa amevaa suti maalum  (Presidential suit) iliyobuniwa na Mbunifu wa mavazi wa Kimataifa kutoka Nchini Tanzania  Sheria Ngowi  akikagua gwaride rasmi kabla ya kuapishwa katika sherehe za kuapishwa kwake jana asubuhi katika viwanja vya National Heroes, mjini Lusaka-Zambia.  Guy Scott, of Scottish      Rais mpya wa Zambia, Edgar Lungu akiwa amevaa suti maalum (Presidential suit)iliyobuniwa na Mbunifu wa mavazi wa Kimataifa kutoka Nchini Tanzania Sheria Ngowi  akila kiapo cha kuwa Rais Mpya wa Zambia  katika sherehe za zilizofanyika  jana asubuhi katika viwanja vya National Heroes, mjini Lusaka-Zambia.  Guy Scott, of Scottish  Rais mpya wa Zambia, Edgar Lungu akiwa amevaa suti maalum (Presidential suit)iliyobuniwa na Mbunifu wa mavazi wa Kimataifa kutoka Nchini Tanzania Sheria Ngowi  akitia saini Hati Maalum Muda mfupi baada ya   kuapishwa katika sherehe za kuapishwa kwake jana asubuhi katika viwanja vya National Heroes, m

MGOMO WA WAENDESHA DALADALA JIJINI MWANZA

Image
Daladala zikiwa zimepaki katika Jiji la Mwanza kutokana na mgomo wa madereva. Taswira kutoka maeneo ya Jiji la Mwanza baada ya mgomo wa waendesha daladala. WAENDESHA magari ya kusafirisha abiria katika ya Jiji la Mwanza maarufu kama daladala leo wamefanya mgomo na kuziba njia zote zinazoingia mjini kutokana na maeneo waliyokuwa wanaegesha magari yao kwa ajili ya kusubiri abiria (stendi) kugawiwa wafanyabiashara ndogondogo maarufu kwa jina la machinga kwa aijili ya shuhuli zao. Daladala zikiwa zimeegeshwa wakati wa mgomo. Hali hiyo imetokea leo asubuhi katika eneo la Stendi ya Tanganyika na Stend ya Soko Kuu jijini Mwanza ambapo yanaegesha magari ya kwenda Airport, Ilemela, Bwiru na Mwaloni ambapo madereva hao waliziba njia zote zinazo ingia kwenye maeneo hayo. Mwenyekiti wa waendesha daladala Mkoani Mwanza, Hassan Dede Petro alisema hali hiyo imejitokeza kutokana na wafanyabiashara hao kuanza kugawana maeneo kwenye stendi hizo bila uongozi wa waendesha daladala

URAIS 2015: JANUARI MAKAMBA VS MWIGULU NCHEMBA NGOMA NZITO!

Image
Naibu Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Teknolojia, January Makamba (41).HOMA ya Uchaguzi Mkuu 2015 inazidi kupanda. Wapo baadhi ya wagombea wa urais ambao tayari wameshatangaza nia hadharani lakini wengine wanaendeleza harakati zao chini kwa chini. Miongoni mwa makada ambao tayari wameonesha nia ya kutaka kugombea ni pamoja na vijana, Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba (40) na Naibu Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Teknolojia, January Makamba (41).  Mwigulu ambaye ni Mbunge wa Iramba Magharibi mkoani Singida, amekuwa na mvuto wa aina yake kisiasa huku akionekana kupendwa zaidi kutokana na kujiwekea nembo yake kwenye mavazi anayovaa kwa kujifunga skafu ya bendera ya taifa.  Mbali na mvuto, Mwigulu tayari alishaanza mizunguko katika majimbo mbalimbali nchini na kuanza kupiga kampeni za ‘kiaina’ ambapo ameonekana kukubalika katika maeneo mbalimbali aliyopita ikiwemo Tanga na Morogoro kabla ya kupigwa ‘stop’ na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana.  Kuonesha

Serikali yafungia gazeti la The EastAfrican

Image
Gazeti la The EastAfrican limepigwa marufuku kusambazwa Tanzania, ikiwa ni miaka 20 baada ya kuanzishwa kwake kwa ajili ya kuandika habari za ukanda wa Afrika Mashariki.   Kwa mujibu wa barua iliyotumwa mwakilishi wa The EastAfrican nchini, uamuzi huo umechukuliwa kwa sababu gazeti hilo “limekuwa likisambazwa nchini bila ya kuwa na usajili, kinyume na kifungu cha 6 cha Sheria ya Magazeti, Namba 3 ya mwaka 1976”.   Uongozi wa Nation Media Group, ambao unamiliki gazeti la The EastAfrican, umeelezea hatua hiyo kuwa ni ya kushangaza na isiyokubalika.   Barua hiyo ya Januari 21, 2015 inaagiza kusimamishwa mara moja kwa uchapishaji na usambazaji wa gazeti hilo nchini Tanzania ‘’hadi litakaposajiliwa rasmi na Msajili wa Magazeti, Idara ya Habari’’.   Kabla ya kutolewa kwa barua hiyo, mwakilishi wa gazeti hilo nchini, Christopher Kidanka aliitwa Jumatano na kuhojiwa na mkurugenzi wa Idara ya Habari, ambaye pia ni msemaji wa Serikali, Assa Mwambene.  

Mshindi wa BBA 2014,Idris Sultan Kanunua Nyumba ya maana maeneo ya Mbezi Beach Dar....Picha zote ziko hapa

Image
Tanzania kupitia Idris Sultan ilibuka mshindi wa shindano la Big Brother Afrika 2014, kwenye interview nyingi alizofanyiwa Idris alisema pesa nyingi atatumia kusaidi watoto Tanzania na Africa.   Habari mpya ni kwamba super star huyu ametumia kiasi flani cha pesa zake kununua jumba lililopo Dar es salaam maeneo ya mbezi Beach.    

Sakata la Escrow: Profesa Muhongo ajiuzulu, asema yeye ni mtu safi, soma kwa kirefu hapa

Image
Waziri wa Nishati na Madini, Mhe. Prof. Sospeter Muhongo akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano aliouitisha leo hii ofisini kwake, ametangaza kujiuzulu wadhifa wake wa Uwaziri baada ya kutuhumiwa kuwa yeye ndiye tatizo linaloendeleza malumbano baina ya Serikali na Bunge kuhusu fedha za akaunti ya Tegera Escrow.   “Nimejiuzulu bila kushinikizwa na mtu yeyote. Mimi ndiyo nitamaliza mjadala huu wa sakata la escrow, nchi ina mambo mengi ya kitaifa yanayotakiwa kujadiliwa lakini watu wamekazana na escrow.    "Nimemuandikia Rais barua rasmi ya kujiuzulu wadhifa wangu. Nimemuomba rais kuachia ngazi ili niipe nafasi serikali yangu kufanya kazi... Nitaendelea kuwa mbunge na mshauri.    “Sidhani kwamba cheo cha mtu mmoja cha uwaziri ni muhimu kuliko hawa masikini ambao wanateseka mchana na usiku.Kwa hiyo nimesema ni sehemu ya suluhisho.   “Nimemuomba Mheshiwa Rais kwamba tafadhali naomba niachane na nafasi ya Uwaziri kusudi taifa lisengo mbele.Hakuna

Kauli ya Zitto Kabwe baada ya Waziri wa Nishati na Madini Ndugu Sospeter Muhongo Kujiuzulu

Image
Kufuatia hatua  ya Waziri wa Nishati na Madini Ndugu Sospeter Muhongo kujiuzulu katika  nafasi  hiyo ya  uwaziri,  mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali Mh Zitto Kabwe amepongeza uamuzi huo wa Prof Muhongo ambapo amesema kuwa hatua hiyo ni heshima kubwa kwa bunge.   "Napenda kuchukua nafasi hii kutambua busara aliyochukua ambayo naamini itasaidia harakati za kujenga demokrasia yenye uwajibikaji.    "Naamini uamuzi wa Ndugu Muhongo umewezesha kulinda heshima ya Bunge na maazimio yake. Kwa muda mfupi alioongoza Wizara hiyo, Ndugu Muhongo ameweza kuongoza mabadiliko kadhaa muhimu ya kiutendaji katika wizara hiyo na taasisi zake.    "Hata hivyo, nafasi ya Wizara aliyokuwa anaongoza katika suala la Tegeta Escrow imemtia doa kubwa ambalo ilikuwa lazima awajibike.    "Naamini Rais Kikwete atamteua mtu mchapakazi na makini zaidi atakayeweza kuendeleza yale mazuri ya Ndugu Muhongo na kurekebisha mapungufu yaliyoj

ANGALIA MABADILIKO MADOGO YA BARAZA LA MAWAZIRI ALILOFANYA RAIS KIKWETE

Image
Wakati aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo ametangaza kujiuzulu nafasi hiyo jana mchana, Rais Jakaya Kikwete ametangaza marekebisho ya Baraza lake la Mawaziri. Akitangaza mabadiliko ya mawaziri hao, Katibu Mkuu Kiongozi wa Ofisi ya Rais,  Ombeni Sefue alitaja mawaziri hao wapya ambao wameapishwa jana jioni na wizara zao kwenye mabano kuwa ni: George Simbachawene (Nishati na Madini), Mary Nagu (Mahusiano na Uratibu), Dk. Harrison Mwakyembe, (Afrika Mashariki). Wengine ni Wiliam Lukuvi (Ardhi, Nyumba na Makazi), Steven Wassira (Kilimo Chakula na Ushirika), Samwel Sitta (Uchukuzi), Jenista Mhagama (Sera na Uratibu wa Bunge) na Christopher Chiza (Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji na Uwezeshaji). Rais pia ameteua manaibu waziri na wizara zao kwenye mabano kama ifuatavyo: Steven Masele (Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano), Angellah Kairuki (Ardhi Nyumba na Makazi), Ummy Mwalimu (Katiba na Sheria), Anna Kilango Malecela (Elimu na Mafunzo ya Ufundi), C

Watu wawili wamefariki Dunia na wawili kujeruhiwa katika matukio mawili tofauti

Image
Mawili tofauti ambapo katika tukio la kwanza maria hauule  mkazi wa Kijiji cha muhukuru songea vijijini mkoani ruvuma  ameuawa kwa kukatwa na shoka kichwani  na mume wake itwaye  salvatory ndimbo  na kasha mwili wake  kuutupa mto mkurumo. Hayo yamesemwa na kamanda wa polisi wa mkoa wa ruvuma ACP Mihayo Msikhela Kamanda mihayo anasema chanzo cha  mauaji hayo ni ugomvi  wa kimapenzi ambapo marehemu maria haule mwenye miaka arobaini  alikuwa na uhusiano wa kimapenzi  na mwanaume mwingine aitwaye  anzekula na kutaka kuachana na  mumewe  salvatory ndimbo mwenye miaka sitini.   Jeshi la polisi linaendelea kumsaka mume wa  marehemu maria Bw. Ndimbo mbaye ametoroka baada ya kufanya unyama huo.   Katika tukio jingine kamanda mihayo amesema kuwa mwendesha bodabodan aitwaye haridi alifa amefariki dunia na watu wawili kujeruhiwa baada ya kugongwa na gari  yenye namba T934BTE,Toyota Mark TU lililokuwa likiendeshwa na mweka hazina wa CCM mkoa wa ruvuma Bw. Silimu

Jeshi la Polisi limekamata shehena ya nyaya za umeme kwenye nyumba ya mkazi mmoja eneo la Nyeburu wilayani Ilala.

Image
Jeshi la Polisi usiku wa kuamkia leo limekamata shehena ya nyaya za umeme kwenye nyumba ya mkazi mmoja eneo la Nyeburu kata ya Majohe wilayani Ilala. Hatu ya kukamatwa na nyaya hizo imetokana na baadhi ya wasamaria wema kuiarifu polisi baada ya kutilia shaka roli moja lililobeba nyaya hizio katika nyumba ya mkazi huyo na kusafirishwa na ndipo polisi ilipofika na kufanya ukaguzi ikazikuta rundo hilo huku mhusika akikimbia na kuacha familia yake.   Meneja wa shirika la ugavi la umeme tawi la kisarawe madaraka marumbo amesema ni wizi mkubwa ambao unashangaza kuona vifaa vilivyokutwa hapo ni vingi vyenye kama ghala huku ikiwa na thamani isiyopungua milioni 100 ambayo vinaweza kupelekwa kwenye mradi wowote.   Mwenyekiti wa mtaa huo wa Nyeburu Bw,Hamisi Gea amesema aliitwa na polisi waliokuwa wakitaka kufanya upekuzi na alishangazwa kuona mkazi huyo ana rundo la vifaa hivyo.   Hadi ITV ikiondoka eneo hilo tayari roli tatu za Tanesco ikiwamo winchi il

Samaki Wa Ajabu Agundulika Ziwa La Victoria

Image
Rare and terrifying frilled shark catch in Victorian waters the first for fishermen in local living memory The hideous, mildly terrifying and rarely sighted frilled shark has turned up in waters off south-eastern Victoria. The species, whose ancestry dates back 80 million years, is known as the 'living fossil'. It was caught on a fishing trawler in waters near Lakes Entrance in the state's Gippsland region. Simon Boag, from the South East Trawl Fishing Association, said it was the first time in living memory that a frilled shark had been sighted. "We couldn't find a fisherman who had ever seen one before," he said. "It does look 80 million years old. It looks prehistoric, it looks like it's from another time!" He said local fishermen were left scratching their heads at the sight of the two-metre-long creature, whose head and body resemble an eel, but whose tail is more reminiscent of a shark. The CSIRO confi

Ajuza miaka 90: anasoma darasa la nne

Image
Gogo akiwa darasani na wanafunzi wenziwe. Akiwa na umri wa miaka 90 mwanamke wa Kenya ambaye anahudhuria masomo akiwa na wajukuu zake wapatao sita inaaminika ndiye mwanafunzi mzee zaidi anayesoma shule ya msingi duniani. Akiwa ameketi dawati la mbele kabisa darasani ,yuko darasa la tano na amevalia nguo za shule , Priscilla Gogo Sitienei anamsikiliza mwalimu anayefundisha kwa makini hukua akiandika majina ya wanyama kwa kiingereza kwenye daftari lake. Prissilla alijiunga na shule hii ya Leaders Vision Preparatory School miaka mitano iliyopita lakini pia aliwahi kuwahudumia wakaazi wa kijiji chake cha Ndalat kilichoko kwenye bonde la ufa kama mkunga miaka sitini na mitano iliyopita. Darasani Priscilla anawasaidia wengine wafanye vyema ambao wana umri kati ya miaka 10 hadi 14 na mar azote huwaambia ujumbe wake hasa mabinti kuwa elimu ndiyo urithi wao. Priscilla anajulikana kama Gogo maana yake bibi katika lugha ya jamii ya wakalenjini,anasefurahia masomo akiw

WANANCHI WAMFANYIA VURUGU MWENYEKITI WA MTAA WA KIGOGO FRESH ANAYEDAIWA KUTAKA KUAPICHWA KINYEMELA

Image
Askari wa Kikosi cha Kutulia Ghasia (FFU), akijaribu kumwokoa mtu aliyejulikana kwa jina la Mariano Haruna baada ya kupewa msukosuko na wananchi wenye hasira , ambaye alidaiwa kuletwa kuapishwa kinyemela kama Mwenyekiti wa Mtaa wa Kigogo Fresh Kata ya Pugu (CCM),  wakati wa zoezi la kuwapisha lililofanyika jijini Dar es Salaam Haruna akiondolewa katika ofisi za Manispaa ya Ilala.

MAKINDA AONGOZA KAMATI YA UONGOZI YA BUNGE, KIKAO CHA BUNGE KUANZA JANUARI 27

Image
Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa Zitto Kabwe akifafanua jambo mbele ya wajumbe wa Kamati ya Uongozi wakati kamati hiyo ilipokaa kuapanga ratiba ya Mkutano wa Bunge kwenye ofisindogo za bunge jijini Dar es Salaam, leo Alhamisi Januari 22, 2015. Kikao cha bunge kinatarajiwa kuanza Januari 27, 2015 Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akiongoza kamati Uongozi leo Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa, Rajabu Mbarouk akieleza jambo mbele ya wajumbe wa Kamati ya Uongozi wakati kamati hiyo ilipokaa kuapanga ratiba ya Mkutano wa Bunge unaoanza jumanne tarehe 27 Januari Mkutano wa Kumi na Nane wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, unatarajiwa kuanza Jumanne tarehe 27 Januari 2015 mjini Dodoma na kumalizika tarehe 7 Februari 2015 Shughuli zitakazokuwepo katika Mkutano huo ni kama ifuatavyo: 1.0 KIAPO CHA UTII Kwa mujibu wa Kanuni ya 24, katika Mkutano wa Kumi na Nane wa Bunge kutakuwa na Kiapo cha Utii kwa Mbunge ambapo Mwanasheria 

POLISI WAWAOKOA MAJAMBAZI WALIONUSURIKA KIFO ZANZIBAR

Image
Mtuhumiwa wa ujambazi akiwa ndani ya gari ya Polisi baada ya kupata kipigo kutoka kwa Wananchi wenye hasira wakati wakiwa katika harakati za kutaka kukimbia jirani na skuli ya darajani baada ya kutelekeza gari waliokuwa wakiitumia aina ya Noah. Mmmoja watuhumiwa wa ujambazi katika maeneo ya darajani akiwa chini ya ulinzi wa Polisi akiwa katika gari waliokuwa kulitumia kwa ujambazi huo.aina ya Rav4.

Picha Pamoja na habari kwa Kina kuhusiana na Majambazi yaliyovamia kituo cha Polisi Ikwiriri na Kuua Askari Wawili na kupora Bunduki

Image
Askari wawili wa Jeshi la Polisi katika Kituo cha Ikwiriri wilayani Rufiji mkoani Pwani, wameuawa baada ya kushambuliwa kwa silaha na majambazi, waliovamia kituo hicho na kuiba silaha baada ya kufanikisha mauaji.   Kutokana na tukio hilo, Jeshi la Polisi liko katika msako mkali, huku Mkuu wa jeshi hilo, IGP, Ernest Mangu akitangaza donge nono la Sh milioni 20 kwa watakaofanikisha kukamatwa kwa wahusika wa tukio hilo na silaha.   Akizungumza na waandishi wa habari kwa njia ya simu kutoka eneo la tukio, Ikwiriri, Kamanda wa Polisi mkoani Pwani, Ulrich Matei alisema majambazi hao walitumia silaha kuwaua askari hao.   Kamanda Matei alisema kuwa tukio hilo lilitokea majira ya saa 8 usiku katika kituo hicho cha Polisi cha Ikwiriri. Aliwataja askari waliokufa kuwa ni mwenye namba E 8732 Koplo Edgar Milinga na WP 5558 Konstebo Judith Timothy.   Alisema licha ya kufanya mauaji hayo, pia majambazi hayo yalipora silaha tano za moto aina mbalimbal