MAMA AJIFUNGUA, MANESI WADAIWA KUMTUMBUKIZA MTOTO KWENYE NDOO


Katoto kachanga kalikotumbukizwa kwenye ndoo kwa zaidi ya saa 3.No! Manesi wa wodi ya wazazi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro wameingia kwenye kashfa nzito ya kusababisha kifo baada ya kudaiwa kumtumbukiza mtoto mchanga kwenye ndoo kwa zaidi ya saa 3. 
Tukio hilo ambalo kwa sasa ni gumzo mkoani hapa lilijiri hivi karibuni ambapo mwanamke aitwaye Zainabu lsmali, mkazi wa Kididimo jirani na Chuo Kikuu Cha Kilimo Cha Sokoine ‘SUA’ alishikwa na uchungu wa kujifungua na kukimbizwa katika hospitali hiyo kwa msaada wa jirani yake aliyejitambulisha kwa jina la Mama Sira Manga.

Ndoo iliyotumika. Akizungumza na Ijumaa Wikienda juu ya tukio hilo, Mama Manga alikuwa na haya ya kusema: “Huu ni uzembe mkubwa wa manesi. Tulipofika hospitali mtoto alizaliwa akiwa hai lakini alikuwa njiti kwani alikaa tumboni kwa mama yake miezi 7 badala ya 9.

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini