BASI LA DAR EXPRESS LAKAMATWA NA MIRUNGI KITUO CHA CHEKERI KOROGWE LIKITOKEA ARUSHA

  Askari wa Jeshi la Polisi wakifanya ukaguzi wa Basi la Dar Express lenye namba za usajili T 244 BXQ.Askari hao wamekamata magunia zaidi ya 16 ya Mirungi katika kituo cha ukaguzi cha Chekeri Korogwe basi ilo lilikuwa linatokea Arusha. Basi hilo lilikamatwa jana majira ya saa nane mchana na kupelekwa mpaka katika kituo cha wilaya cha Polisi Korogwe, Mtu mmoja anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa kuhisiwa anahusika na tukio hilo pia konda wa Basi hilo anashikiriwa na Polisi. 
Askari wa Jeshi la Polisi wakiwa wanapakia Magunia ya Mirungi katika Gari lao.Endelea kufuatilia hapa Taarifa kamili.CHANZO: TANGA YETU BLOG

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini