AJALI YAUA ZAIDI YA 50 NCHINI PAKISTAN

Basi likiwa limeteketea baada ya ajali hiyo.
Taswira kutoka ndani ya basi hilo la abiria.
Baadhi ya miili katika ajali hiyo ikiwa Hospitali ya Jinnah, Karachi.
WATU zaidi ya 50 wamefariki dunia huku wengine kadhaa wakijeruhiwa baada ya basi la abiria kugongana na lori la mafuta kisha magari yote kuteketea kwa moto jirani na Mji wa Karachi nchini Pakistan.
Imeelezwa kuwa lori la mafuta lilikuwa katika spidi kali lilipogongana uso kwa uso na basi hilo.
Basi lilikuwa limebeba watu zaidi ya 60 na lilikuwa likielekea kwenye Mji wa Shikarpur kutokea Karachi.
Dk. Seemi Jamali, mkuu wa kitengo cha dharura katika Hospitali ya Jinnah mjini Karachi amesema kuwa wamepokea miili ya watu 57 huku akiongeza kuwa idadi inaweza kuongezeka.
Chanzo: BBC

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini