WANAFUNZI 150 WA CHUO KIKUU CHA DUCE WADUNGWA MIMBA

Wanafunzi 150 kati ya 1,000 waliojiunga na masomo katika Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) mwaka jana wamebainika kuwa na ujauzito waliopewa na wenzao chuoni hapo.
Utafiti wa usawa na jinsia uliofanywa na chuo hicho kati ya Juni na Novemba mwaka jana umebaini kuwa wanafunzi wanaopata ujauzito ni wale wa mwaka wa kwanza.

Hayo yamebainishwa jana na Mratibu wa Masuala ya Jinsia wa chuo hicho, Dk Dativa Shilla katika warsha ya uchaguzi na uhusiano wa kijinsia iliyofanyika chuoni hapo na kusema hali hiyo inatokana na kuwapo kwa vitendo vya ukatili, manyanyaso na ubabe unaofanywa na wanachuo wa kiume dhidi ya wale wa kike na hivyo kuwalazimisha kufanya mapenzi bila hiyari yao.
“Kupitia utafiti huu tumeona hakuna usawa wa kijinsia wa kupata elimu baina ya mwanamke na mwanamume kwa sababu mwenye ujauzito hawezi kufanya vizuri katika masomo yake ukilinganisha na mhusika wa kiume,” alisema.
Mwanafunzi wa mwaka wa pili katika chuo hicho Gosbeth Kihanga ambaye alikiri kuwapo kwa vishawishi chuoni hapo na kudai kuwa inachangiwa na ugumu wa maisha hasa kwa wanafunzi wa kike.

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini