Mwandishi aliyetuhumiwa kwa Rushwa aachiwa huru


MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Arusha, jana imemwachia huru aliyekuwa Mhariri wa Gazeti la Rai, Masyaga Matinyi baada ya kushindwa kumtia hatiani dhidi ya tuhuma za kupokea rushwa zilizomkabili yeye na wenzake watatu.

Pia Mahakama hiyo imemtia hatiani mtuhumiwa wa pili Mwita Chomete na kumhukumu kifungo cha mwaka mmoja jela au kulipa faini ya Shilingi laki tatu.
 
Katika kesi hiyo ya Mwaka 2012 mlalamikaji alikuwa Andrew Meza akisaidiwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), dhidi ya Matinyi, Chomete na Bora Bidige wanaodaiwa kushawishi na kupokea rushwa wilayani Monduli mkoani Arusha. 
 
Akisoma hukumu hiyo mapema leo, Hakimu wa mahakama hiyo, Gwantwa Mwankuga amesema, katika kosa la kwanza Mahakama, imeshindwa kuwatia hatiani watuhumiwa wote kutokana na upande wa mlalamikaji kuwasilisha ushahidi mwepesi.
 
Katika upande wa walalamikaji waliwasilisha mashahidi Saba, huku mashahidi katika shitaka la kushawishi wakiwasilisha ushahidi wa mawasiliano ya simu ambayo yalidaiwa kuwa si rasmi kutoka kwenye mamlaka zinazohusika na mawasiliano.
 
Kutokana na uamuzi huo Mahakama hiyo iliwakuta hawana hatia watuhumiwa wote watatu, katika kosa hilo la kwanza hivyo kuwaachia huru Matinyi, Chomete na Bigide.
 
Akisoma shitaka la pili liliwakabili pia watuhumiwa wote Hakimu Gwantwa, amesema, mtuhumiwa wa pili Chomete alikutwa na hatia katika kosa hilo kutokana na ushahidi wa mashahidi wa kwanza na wa pili kueleza kuwa alipokea rushwa ya fedha.
 
Amesema katika ushahidi wa mashahidi wa kwanza na wa pili, wameeleza kwamba mtuhumiwa wa pili alipokea fedha japo hawakuthibitisha zilikuwa ni fedha za nini.
 
Gwantwa amesema kwa maana hiyo, kitendo cha fedha kutupwa nje kinathibitisha wazi kwamba fedha ilitolewa ndani. hivyo Mahakama imemtia hatiani kwa kifungo cha mwaka mmoja jela au faini ya Shilingi laki tatu.
 
Hata hivyo mtuhumiwa wa pili Chomete aliyekutwa na hatia, amelipa faini ya Shilingi laki tatu na kuachiwa huru.
 
Katika kesi hiyo Matinyi alikuwa akitetewa na Wakili Mwandamizi wa jijini Arusha Moses Mahuna, kutoka Kampuni ya Law Acces Advocates.
 
Akizungumzia mara baada ya kushinda kesi hiyo nje ya mahakama hiyo, Matinyi amemshukuru Mungu na kumpongeza wakili wake kwa kumpigania

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini