Posts

Showing posts from October, 2015

Profesa KITILA MKUMBO Ampa Ushauri Huu Edward LOWASSA Kuhusu Matokeo!

Image
Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa Kitila Mkumbo amesema aliyekuwa mgombea wa urais wa Chadema, Edward Lowassa, hana budi kukubali matokeo licha ya kupoteza nafasi hiyo. Pia Profesa Mkumbo alisema mgombea huyo kisheria, hakuwa na haki ya kujitangaza mshindi wa nafasi ya urais katika uchaguzi wa mwaka huu. Juzi, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ilitangaza matokeo ya kura za urais zilipopingwa Jumapili, Oktoba 25 mwaka huu na kumtangaza mgombea wa urais kwa tiketi ya CCM, Dk John Magufuli mshindi, lakini Lowassa siku hiyo pia alisema ameshinda katika uchaguzi kwa kura 10,268,795 sawa na asilimia 62 na kuitaka tume hiyo kumtangaza mshindi. Profesa Mkumbo ambaye pia alipendekezwa na chama cha ACT- Wazalendo kugombea nafasi hiyo na kukataa, alisema Lowassa aliingia kwenye kinyang’anyoro hicho akifahamu kuwa tume ndiyo yenye mamlaka ya kumtangaza mshindi. Alisema licha ya mchuano mkali kati yake na mgombea wa CCM anatakiwa kukubali matokeo. “Hivyo

UKAWA Watoa Tamko Zito Lenye Masharti Manne

Image
Viongozi wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), wamesema baada ya kufuatilia mwenendo wa Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar wana taarifa za uhakika kwamba Maalim Seif Sharif Hamad, Mgombea Urais wa Chama cha Wananchi (Cuf) anayeungwa mkono na Umoja huo, ameshinda urais wa Zanzibar. Taarifa iliyotolewa na viongozi hao jana kwa vyombo vya habari imetoa masharti  manne kufuatia kufutwa kwa uchaguzi wa Zanzibar. Sharti la kwanza  ni kuzitaka mamlaka zinazosimamia Uchaguzi Mkuu huo kuondoa mara moja tangazo la kuufuta Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar.   Sharti la pili  ni kumtangaza Seif kuwa ni mshindi halali wa nafasi ya urais na hivyo aapishwe kuwa Rais wa nchi ya Zanzibar ambayo ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.   Sharti la tatu,  wametoa  wito kwa Jumuiya ya Kimataifa kuingilia kati na kulaani kwa nguvu zote kinachofanyika Zanzibar ambako kwa mara nyingine tena demokrasia inataka kuminywa wazi wazi  ili tu kuinusuru CCM isiondoke madarakani kama

Hali ni Tete Zanzibar....Bomu Lategwa Kituo cha Polisi, JWTZ Waliwahi na Kulilipua!

Image
Jeshi la Polisi Zanzibar kwa kushirikiana na Jeshi la Wananchi (JWTZ), limefanikiwa kuteguwa bomu lilitegwa eneo la Mkunazini karibu na kituo cha polisi mjini Zanzibar. Bomu hilo lilitegwa na watu wasiofahamika na jeshi la polisi lilipata taarifa ya kutegwa kwa bomu hilo kutoka kwa wasamaria wema. Akizungumza na mwandishi wetu, Kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar, Hamdani Omar Makame, alisema baada ya kupata taarifa kutoka kwa wananchi kuwa eneo hilo kuna kitu kimetegeshwa, jeshi la polisi lilifanya uchunguzi na kubaini kuwa ni bomu na kufanikiwa kulitegua kwa kuliripua ili kuepusha maafa. “Ni kweli kulikuwa na kishindo kikubwa baada ya jeshi la polisi kuliripua bomu hilo lakini hakuna madhara yoyote yaliotokea,” alisema. Aidha alisema kuwa jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi ili kubaini ni aina gani ya bomu lililotegwa na aliyefanya kitendo hicho.

WIZKID Atua Dar, Tayari Kwa Shoo Yake Leaders Leo [+PICHAZ]

Image
Wizkid baada ya kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) usiku huu. Wizkid akisindikizwa na walinzi mara baada ya kuwasili Dar usiku huu. Warembo wakisubiri kumpokea Wizkid. Wizkid akiongea na wanahabari waliofika kumpokea usiku huu. Wizkid akielekea kwenye gari tayari kwa safari ya kuelekea hotelini. Gari lililombeba Wizkid. MWANAMUZIKI mahiri kutoka nchini Nigeria, Ayodeji Ibrahim Balogun maarufu kama Wizkid ametua nchini usiku huu tayari kwa onyesho lake litakalofanyika hapo baadaye kwenye Viwanja vya Leaders jijini Dar es Salaam.   Staa huyo amewasili nchini majira ya saa 7 na kuwasalimia mashabiki wake waliofika uwanjani hapo kumpokea huku akitoa maneno ya utani kuwa amekuja kuwaona warembo wa Tanzania. Wizkid ambaye anafanya vizuri kwa wimbo wake wa Ojuelegba atafanya onyesho kubwa la kihistoria Afrika Mashariki, chini ya usimamizi wa Kampuni King Solomoni Entertainment.   Msanii

Rais JAKAYA KIKWETE Anatuacha Pazuri -JB

Image
Staa wa Bongo Movie, Jacob Steven JB akisalimiana na rais  Jakaya Kikwete. MKONGWE kwenye sanaa ya filamu Bongo, Jacob Stephen ‘JB’ amefunguka kuwa rais wa awamu ya nne anayemaliza muda wake, Jakaya Kikwete anaondoka madarakani akiwa ametoa msaada mkubwa sana katika sanaa.   Akizungumza na mwanahabari wetu hivi karibuni, JB alisema Rais Kikwete alikuwa akitoa msaada mkubwa sana kwa wasanii ikiwemo kushiriki katika masuala yao ambayo uwepo wake tu ulitosha kuifanya sanaa izidi kujulikana na kupiga hatua. “Kikwete ametoa ushauri wa mawazo. Amekuwa akishirikiana nasi katika shida na raha. Kutuzungumza tu katika hadhara kwetu sisi ni jambo kubwa, tutamkumbuka kwa mengi sana,” alisema JB.

Mrembo Amburuza DUDE Polisi! Kisa Nimekuwekea Hapa...

Image
Mrembo anayedai kuzaa na mwigizaji Kulwa Kikumba ‘Dude’, Ester Eliakim akiwa na mtoto huyo.   GLADNESS MALLYA   MREMBO anayedai kuzaa na mwigizaji Kulwa Kikumba ‘Dude’, Ester Eliakim amekwenda polisi, Kituo cha Stakishari kumshtaki mwigizaji huyo akidai hampi matumizi ya mtoto anayedai kuzaa naye. Mwigizaji Kulwa Kikumba ‘Dude’.   Licha ya Dude kumkana motto huyo, mrembo huyo amesema ana uhakika mtoto huyo amezaa na Dude lakini kinachomsikitisha kila anampomuomba matumizi, staa huyo amekuwa akimtukana badala ya kumjibu vizuri. “Nimempeleka polisi pale Stakishari. Nikapelekwa Dawati la Jinsia. Amepigiwa simu ya kuitwa akadai hayupo Dar na kuahidi akirudi atafika ili tutafute muafaka,” alisema Ester.   Alipotafutwa Dude kuhusiana na ishu hiyo, aliendelea kusisitiza kwamba hamtambui mrembo huyo bali anataka kujitafutia umaarufu kupitia jina lake. “Nilishasema simjui huyo mtu bwana, aniache, atakuwa anatafuta umaarufu tu,” alisema Dude.

MADAI MAZITO: Nyumba ya DIAMOND si Yake! Ukweli Huu Hapa....

Image
Nyumba ya Diamond inayodaiwa si yake.   GLADNESS MALLYA IMELDA MTEMA IMEVUJA! Ile nyumba ya kifahari iliyoaminika ni ya staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ imefahamika kuwa siyo yake kama wengi walivyokuwa wakifahamu. Diamond Platinumz. Kuvuja kwa siri hiyo kumetokana na maneno ya wambeya yaliyokuwa yakielekezwa kwa mama mzazi wa staa huyo, Sanura Kasimu ‘Sandra’ mitandaoni kwamba kwa nini asiondoke kwenye nyumba hiyo na kumuacha mwanaye awe huru ndipo mwanahabari wetu alipomtafuta mama Diamond na kumuuliza kuhusu maoni ya wambeya hao, bi. mkubwa huyo akasema hawezi kuondoka kwani nyumba hiyo siyo ya Diamond bali ni mali yake. Nyumba ya Diamond inayodaiwa si yake. “Kwa taarifa yenu hii nyumba ni ya kwangu na makaratasi yote yameandikwa jina langu hao wanaosema nimwache Nasibu awe huru hawajui lolote, mimi ndiyo nimesimamia kila kitu na Nasibu hakuwahi kusimamia hata siku moja, hii ni nyumba yangu. “Wanaosema awafukuze ndugu zake nawaambia kwamba hapa ha

FAINALI Ligi ya Mabingwa Afrika Leo: Mtanzania MBWANA SAMATTA Anaweza Kuweka Rekodi Hii....

Image
Michuano ya fainali ya klabu Bingwa  Afrika  inatarajia kufanyika leo October 31 nchini Algeria  kwa mchezo wa kwanza wa fainali hiyo kupigwa, huu ni mchezo ambao hisia za watanzania wengi wamezielekeza huko kwa kuwatazama mastaa wa soka wa Tanzania  ambao wanatazamiwa kucheza katika mechi hiyo  Samatta  na  Ulimwengu .   Mchezo wa fainali ya Ligi ya Mabingwa  Afrika  unachezwa leo October 31 kwa kuzikutanisha timu za  US Alger  ya  Algeria  dhidi ya  TP Mazembe  ya Jamhuri ya kidemokrasia ya  Kongo  ambayo inachezewa na watanzania wawili  Mbwana Samatta  na Thomas Ulimwengu , stori ni kuwa  Mbwana Samatta  huenda akaweka rekodi ya kuwa mfungaji bora wa michuano hiyo kwani hadi sasa ana goli 6 hivyo kama atafanikiwa kufunga katika mechi mbili za fainali anaweza twaa tuzo ya mfungaji bora. Klabu ya  TP Mazembe  imewahi kutwaa klabu Bingwa  Afrika  mara nne wakati wapinzani wao  US Alger  hawajawahi kutwaa Kombe hilo hata mara moja, hivyo kila timu inaingia uwanjani

DONDOO MUHIMU Kuhusu Rais Mteule DK MAGUFULI Kuanza Kazi!

Image
Rais Jakaya Kikwete (kushoto) na rais mteule wa awamu ya tano, Dk John Pombe Magufuli (kulia). ISSA MNALLY NA RICHARD BUKOS JANA, aliyekuwa mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Pombe Magufuli (56) alikabidhiwa cheti cha kuutambua ushindi wake wa nafasi hiyo baada ya kuibuka na kura nyingi kwenye uchaguzi uliyofanyika Oktoba 25, mwaka huu huku watu wakisema kitendo cha kumkabidhi cheti kazi imeanza. Rais mteule wa awamu ya tano, Dk John Pombe Magufuli akionesha cheti cha ushindi wa urais kwa aliyekuwa mgombea wa urais kwa tiketi ya chama cha ACT-Wazalendo, Mghwira. Hafl a ya kumkabidhi cheti Magufuli ilifanyika kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar kuanzia saa nne asubuhi na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali, waangalizi wa kimataifa (akiwemo rais mstaafu wa Nigeria, Gudlucky Jonathan), pia wakiwemo waliokuwa wagombea wengine wa nafasi ya urais. Viongozi waliohudhuria ni rais anayemaliza muda wake, Jakaya Kikwete ‘JK’, Spika wa Bunge, A

ALICHOKIANDIKA MGOMBEA URAIS TOKA ACT KUHUSU USHINDI WA DK MAGUFULI

Image

SUMAYE Na Kisa Cha Mchimba Kisima!

Image
Ndugu zangu, Fredrick Tluway Sumaye ni mmoja wa walioshindwa sana kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka huu. Ni heri ya Lowassa na Kingunge kulikoni Sumaye. Nilibaki nikimshangaa Sumaye aliposimama majukwaani na kuiponda CCM huku akilaumu pia Katiba inayovikandamiza vyama pinzani. Katika uchaguzi wa mwaka huu yumkini wapiga kura wamewaadhibu watu wa aina ya Sumaye na kuwaonyesha, kuwa wao wapiga kura si wajinga. Nilimshangaa Sumaye na Kingunge kusimama majukwaani na kulaumu mfumo ambao wao walishiriki kuujenga na kuulinda. Kwa Sumaye na Kingunge wanapolaumu Tume ya Uchaguzi na Katiba ya Nchi ya mwaka 1977 wanasahau, kuwa wao wakiwa madarakani walikuwa na nafasi ya kuweka mazingira ya kufanyiwa mabadiliko. Ona Fredrick Sumaye, ukiacha mapendekezo ya Jaji Francis Nyalali ya mwaka 1992 ambayo yaliainisha sheria 40 kandamizi, na hata Sumaye alipoteuliwa kuwa Waziri Mkuu mwaka 1995, sheria hizo 40 kandamizi alizikuta, hakufanya lolote. Mwaka 1998, Ben Mkapa aliunda Tume ya Jaji Kissanga i

KISHANUKA TAYARI....Kujiuzulu kwa MBOWE na Mustakabali wa CHADEMA

Image
Kwa kweli nimesikitishwa sana namna chama mahiri cha upinzani kama CDM kudhalilika kiasi hiki katika uchaguzi huu mkuu. Niliipenda CDM-Asilia lakini ilipoingiliwa na wana CDM-Maslahi niliamua kuitosa na kumpigia debe Magufuli. Uchaguzi umekwisha na tunae Raisi.   Je Tunao Upinzani Mahiri Tena? Kwa kweli CDM imeathirika sana na inaweza kumeguka vipande vipande. Kwa sasa naona ACT-Wazalendo wanaweza kupata wafuasi wengi sana na kuwa chama kikuu cha upinzani ifikapo 2020. Sidhani kama tuna upinzani mahiri tena kwa sasa. CDM Wafanye Nini Sasa: Cha kwanza ni kumng'oa haraka sana yule rubani aliebadilisha gia angani na kukiangamiza CHOMBO. YES, lazima mheshimiwa Mbowe awajibike haraka sana kama wana CDM watakuwa na imani tena na chama chao, la sivyo itakuwa ni mafuriko kuelekea ACT, au CCM. Leadership ethics zinamshinikiza Mbowe aachie kiti. Utabiri wangu uchwara ni kuwa sidhani CDM inaweza kuji-rehabilitate tena katika miaka mitano ijayo. Pengine ni mpaka 2025 ndio wanaweza kuwa

WATU WENGI WAPENDELEA MAGUFULI AMTEUE HUYU AWE WAZIRI MKUU ILI WATU WASILALE MAOFISINI

Image
Rais Mteule Dr John Pombe Magufuli PROFESA SOSPETER MUHONGO  Je, wewe kama mdau wa siasa na mtanzania mzalendo una maoni gani juu ya kiongozi huyu?!

BUSUNGU Aleta Tafrani, Awaondoa Watatu YANGA SC

Image
Wilbert Molandi, Dar es Salaam KUINGIA kwenye kikosi cha kwanza cha Mholanzi, Hans van Der Pluijm, mshambuliaji wa Yanga, Malimi Busungu, kumewapa wakati mgumu viungo wa pembeni, Mbrazili, Andrey Coutinho, Geofrey Mwashiuya na Simon Msuva. Awali, Busungu alikuwa akianzia benchi kwenye kikosi cha Mholanzi huyo ili kuwapisha, Donald Ngoma na Amissi Tambwe kwenye nafasi kabla ya kuhamishiwa pembeni kucheza kama kiungo mshambuliaji. Busungu alianza kuaminika na kuanza kuingizwa kwenye kikosi cha kwanza cha Pluijm wakati timu hiyo ilipovaana na Simba katika mechi ya Ligi Kuu Bara akitokea benchi kuchukua nafasi ya Msuva na kufunga bao katika ushindi wa mabao 2-0 huku lingine likifungwa na Ngoma. Tangu siku hiyo, mshambuliaji huyo alikuwa akipangwa kucheza kiungo wa pembeni kama siyo namba 7 iliyokuwa inachezwa na Msuva, basi 11 waliyokuwa wanapokezana Coutinho na Mwashiuya. Wakati Busungu akicheza nafasi moja ya kiungo wa pembeni, nafasi nyingine ya pembeni wamekuwa wakipangwa H

Alichokiandika Bilionea MENGI Baada ya DK MAGUFULI Kutangazwa Kuwa Rais Mteule wa Tanzania!

Image
Hiki hapa ndicho alichopost bi l ionea Mengi