Joyce KIRIA Alalamika Mumewe Kushindwa Ubunge Kumemkosesha Nyumba Nzuri na Shopping UK

Kupitia account yake ya Instagram, Joyce Kiria amelalamika mumewe kushindwa ubunge na Maghembe kumemkosesha yeye kupata nyumba nzuri na shopping za Ulaya.
Mrekebishatabia
Joyce ni Mdada niliyeamini anaweza kuwa mfano bora kwa jamii kutokana na kazi mbali mbali alizofanya na kujitolea kwa wananchi...nilimwona kama shujaa na mwanamke ambaye hata angesimama kugombea jimboni peke yake angepita bila kupingwa. Nilikuwa na picha ya mwanamama Fulani wa nguvu ambaye ndani ya miaka michache ijayo Tanzania ingeheshimika kupitia yeye.
Lakini nachelea kusema amejiharibia sana mambo mengi wakati huu wa uchaguzi ni pamoja na kutoa lugha chafu mitandaoni akijua kabisa mumewe anagombea vijijini ambako watu hujiheshimu.

Sasa nikajua labda ana uchungu na wananchi ndo maana alikuwa vile kuumbe anawaza safari za ulaya? Yaani kusema ukweli nimekwazika na nahisi aibu kama mimi ndo Joyce. Na siamini nilichokisoma kutoka kwake. Uchaguzi huu umenifanya nimfahamu Joyce vema....na tulisema kuna maisha baada ya uchaguzi...nitaendelea na wengine!!!

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini