Wazazi waliingilia ndoa ya mtoto wao, mkwe akaona alipize kisasi

Migogoro kwenye ndoa wengine wanaona ni kawaida, wengine huwa inawachosha.. Ziko story utasikia wanandoa wamepigana, wengine wanaachana.
Nimeipata hii stori toka India, Rekha Nagvanshi ni mwanamke ambaye ameonekana kuchoshwa na manyanyaso ya mume wake, kuna wakati waliachana.. baadae wakarudiana.
Baada ya kurudiana makubaliano ilikuwa hivi, mume awe anahusika na majukumu yote ya nyumbani yani kuanzia kufua nguo, kuosha vyombo.. kupika.
Wazazi waliingilia kati na kufanya makubaliano hayo yakavunjika, Rekha hakuridhika wazazi kuingilia kati masuala yao ya ndoa.
rekha_650x400_51428053665
Rekha Nagvanshi
Rekha alikutwa na mama mkwe wake akikojolea kwenye birika la chai jikoni, rafiki yake anasema labda kwa vile alikasirishwa na wazazi hao ndio maana akaamua alipize kisasi kwa kufanya hivyo.
Wazazi hao wamesema walikuwa wanajua mkwe wao hawapendi lakini hawakufikiria kama angeweza kuwafanyia kitendo hicho, walienda kutoa taarifa Polisi lakini majibu ya Polisi waliwaambia hawashughulikii kesi za namna hiyo.
Mume wa mwanamke huyo ambaye anaitwa Deepak amesema yeye aliridhika na masharti ya mke wake waliporudiana lakini wazazi wake hawakupenda kuona anafanywa kama mtumwa.

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini