DK MAGUFULI Afunguka Kuhusu Kulazwa ICU!

MgombeaUrais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk John Magufuli, amekanusha madai ya kuugua na kulazwa katika Chumba cha Wagonjwa Mahututi (ICU), Katika Hospitali ya Mkoa wa Mbeya. 
Dk Magufuli alisema hayo jana wakati akishukuru uongozi wa CCM wa mkoa huo, kwa mapokezi mazuri tangu alipoingia katika mkoa huo Alhamisi wiki hii akitokea Rukwa.

Madai ya kuugua na kulazwa kwa Dk Magufuli, yalianzia juzi katika Hospitali ya Mkoa wa Mbeya, alipokwenda kumjulia hali Meya wa Mbeya, Athanas Kapunga, aliyepata ajali Alhamisi wiki hii alipojiunga na msafara wake kwenda Makambako.

Meya huyo alipokuwa akitoka katika kijiji cha Nzoka kwenda Makambako baada ya kumpokea Dk Magufuli, akiwa nyuma ya msafara wa mgombea huyo, gari alilopanda liliacha njia na kupinduka ambapo mtu mmoja aliyekuwa amepewa lifti, alikufa na wengine akiwemo Meya huyo kujeruhiwa.

Kutokana na ajali hiyo, Dk Magufuli kabla ya kuanza ziara yake juzi mkoani Mbeya alikwenda kumjulia hali Meya huyo katika hospitali hiyo, ambako amelazwa Chumba cha Wagonjwa Mahututi (ICU), ndipo kukasambaa uongo huo kwamba amelazwa.

Mbali na kukanusha uvumi huo, Dk Magufuli aliushukuru uongozi wa CCM Mkoa wa Mbeya na wananchi kwa ujumla kwa makaribisho mazuri.

Katika mkoa huo amekuwa akipokewa na maelfu ya wananchi katika mikutano mikubwa na mamia katika mikutano midogo, ambako amekuwa akisimamishwa mara kwa mara na wananchi njiani, ambapo Dk Magufuli alisema mapokezi hayo yameonesha kuwa Watanzania wengi wanataka mabadiliko bora na si bora mabadiliko.

Mbali na shukrani hizo, pia aliupa pole uongozi huo wa CCM Mbeya na wananchi kwa msiba wa kada mmoja wa chama hicho, aliyekufa katika ajali hiyo iliyomjeruhi Meya.

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini