Jaji wa ESCROW Kusikiliza Kesi ya Ubunge wa David KAFULILA

Kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi iliyofunguliwa na aliyekuwa Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila, kupinga matokeo ya uchaguzi itaanza kusikilizwa leo na Jaji John Utamwa katika Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Tabora.

Kafulila aliyekuwa Mbunge kinara katika kuibua ufisadi wa sakata la uchotwaji wa zaidi ya Sh. bilioni 306 katika akaunti ya Tegeta Escrow iliyokuwa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), anakutana ‘uso kwa uso’ na Jaji Utamwa, ambaye ndio alitoa hukumu tata iliyosababisha kuibuka kwa kashfa ya ufisadi wa fedha hizo.

Jaji Utamwa aliitoa hukumu hiyo, Septemba 8, 2013 kwa kumwamuru Kabidhi Wasihi, kukabidhi mtambo wa Kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL) kwa mmiliki wake mpya ambaye ni kampuni ya Pan Africa Power Solutions Tanzania Limited (PAP) baada ya kukubaliana na maombi ya aliyekuwa mbia wa IPTL, kampuni ya Engineering and Marketing Limited (VIP) iliyoondoa kesi yake kwa lengo la kuifilisi IPTL.

Hukumu hiyo ndio ilikuwa chanzo cha Kafulila kuibua kashfa hiyo bungeni kwa kuwahusisha vigogo mbalimbali wa serikali na ufisadi huo.

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini