ODAMA ATESWA NA HOFU YA KIFO!!

 
 Mtoto mzuri Bongo Movies, Jennifer Kyaka ‘Odama’.
MTOTO mzuri Bongo Movies, Jennifer Kyaka ‘Odama’ amefunguka kuwa kadri anavyosherehekea siku yake ya kuzaliwa ndivyo hofu ya kifo inavyozidi kumjaa.

Odama alifunguka hayo juzi alipokuwa akisherehekea siku yake ya kuzaliwa katika Ukumbi wa Vijana ambapo alisema kutokana na hofu hiyo ndiyo maana aliamua kujumuika na watoto yatima.

“Mwenzenu sijui nipoje yaani kila inapofika bethidei yangu najikuta nikiingiwa na hofu ya kifo, bora niwe nasherehekea na watoto yatima kama hivi nipate thawabu kwa Mungu,” alisema Odama.

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini