KIPA PETR CECH ATUKANWA NA KUTISHIWA KUUAWA BAADA YA KUJIUNGA NA ARSENAL...SHUHUDIA HAPA1

 Golikipa mpya wa Arsenal, Petr Cech amepokea vitisho vingi vya kuuawa kutoka kwa mashabiki wanaoaminika kuwa wa Chelsea kupitia mtandao wa Twitter baada ya kutua Emirates kwa dau la paundi milioni 10.

 Mashabiki hao hawajafurahishwa na maamuzi ya Cech kwenda timu nyingine ya London, licha ya ukweli kwamba ameitumikia timu yao kwa heshimu ndani ya miaka 11 aliyodumu Stamford Bridge.  

Watumiaji wengi wa Twitter wanaoaminika kuwa mashabiki wa Chelsea wamemuita Cech ‘Msaliti ‘ na ‘nyoka’, wakati wengine wakisema ‘Cech atakufa kwao, mvaaji wa Helmet ya nyoka”. 
Matusi hayo ya mashabiki kwenye mtandao wa Twitter yamekuja baada ya Cech kujiunga na wapinzani wao wakubwa, Arsenal. 
 
 
 
 
 
Shabiki mmoja wa Chelsea anayetumia jina la ‘@Febreezion’ ameenda mbali zaidi akitweet kwamba: 
“Iage familia yako kwa mara ya mwisho kabla ya kwenda kulala, hutawaona tena kesho, nyoka mkubwa wewe”. 

Mwingine amekumbukiza tukio ambalo lilimfanya Cech apata majeraha makubwa ya kichwa kwa kugongana na kiungo wa Reading, Stephen Hunt mwezi Oktoba 2006.
‘F*** you Petr Cech you fucking snake, can’t believe you went to f***ing Arsenal. Really wish Stephen Hunt ended your life. F***ing C***.’ (Hatujaona haja ya kutafsiri kwa sababu za kimaadili”. 

Tweet hizo za matusi zinazomlenga Cech na familia yake zimeendelea kwa mtu anayeitwa @Enegali10 ambaye amepost: ‘F******** off just saw Cech signed. Go f*** yourself. F****** brain damaged ugly sk**. Hope your kids have cancer. F****** nonce

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini