TAMKO la SERIKALI Kuhusu Taarifa za UHABA wa MAFUTA!

Serikali imekanusha taarifa zinazosambazwa katika mitandao ya kijamii, kuwa kuanzia kesho na keshokutwa kutakuwa na uhaba wa mafuta kwenye vituo vya kuuza mafuta.

 Kauli hiyo ya kukanusha imetolewa na Naibu Waziri wa Nishati na Madini Charles Mwijage wakatia kijibu swali lililoulizwa na Job Ndugai jana Bungeni, Dodoma. 

Ndugai alimtaka Waziri kutoa ufafanuzi kuhusu taarifa ambazo zinasambazwa kwenye mitandao ya kijamii kwamba kaunzia kesho kutakua na tatizo la upatikanaji wa mafuta na kusababisha shughuli nyingi kusimama. 

Mwijage alisema taarifa ambazo wanazo kama Wizara ni kuwa hifadhi ya mafuta ipo ya kutosha na kuwa uhaba wa mafuta hauwezi kutokea kwa kuwa wana uhakika kuwa mafuta yapo ya kutosha. 

Alisema hata yeye ameonakwenye mitandao ya kijamii na sasa wanafuatilia ili kujuab chanzo cha taarifa hizo ni nini.
lisema iwapo kuna msambazaji au mfanyabiashara atajaribu kufanya hivyo kanuni kanuni na sheria zilizopo zitatumika kuhakikisha wahusika wanawajibishwa.

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini