MAJANGA! MWALIMU WA SEKONDARI AKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA ‘UNGA’ PIPI 101 JIJINI DAR

Na Makongoro Oging’

Mwalimu wa shule moja ya sekondari mkoani Singida (jina la shule linahifadhiwa), Charles Andrew (46) amekamatwa na Kikosi Kazi cha Kudhibiti na Kupambana na Madawa ya Kulevya nchini (task force) katika Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere akidawa kuwa na mzigo wa ‘unga’ pipi 101 ya aina ya heroin yenye zaidi ya shilingi milioni mia moja.
 
Mwalimu wa shule moja ya sekondari mkoani Singida (jina la shule linahifadhiwa), Charles Andrew (46) anayedaiwa kukamatwa na unga.
 Taarifa kutoka vyanzo vyetu makini ndani ya kikosi hicho zinasema kwamba mwalimu huyo alikamatwa Juni 25, mwaka huu, saa kumi alfajiri akijianda kusafiri kwenda nchini Ghana kupitia Nairobi.
Habari zaidi zinadai kwamba mwalimu huyo alipokamatwa alikutwa na pipi 40 akiwa amezificha sehemu za siri na baadaye alitoa pipi 61 ambazo alimeza tumboni.


Kamanda wa Polisi Kikosi cha Kupambana na Kudhibiti Madawa ya Kulevya Tanzania, Godfrey Nzowa alipoulizwa ofisini kwake na mwandishi wetu juzi alikiri kukamatwa kwa mtu huyo na kiasi hicho cha madawa.
“Tulipata taarifa kutoka kwa raia mwema ndipo tukaweka mtego na tukafanikiwa kumkamata mtu huyo ambaye kitaaluma ni mwalimu wa shule ya sekondari huko mkoani Singida, hata hivyo tutamfikisha mahakamani wakati wowote upelelezi ukikamilika,” alisema Kamanda Nzowa.
Kamanda Nzowa amewashukuru wananchi kwa ushirikiano wanaotoa juu ya wauza na watumiaji wa unga na waendelee kushirikiana na polisi ili kukomesha kabisa biashara hiyo haramu.

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini