SISTADUU ALIYEVAA KIPENSI AKIONA CHA MOTO JIJINI DAR!

Sistaduu mmoja ambaye hakufahamika jina lake ila ni mkazi wa Temeke jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki iliyopita alionja joto ya jiwe kufuatia kuvaa kipensi kilichoacha sehemu kubwa ya mwili wake kuwa wazi.

Tukio hilo lilijiri Jumamosi iliyopita eneo la Temeke Hospitali baada ya dada huyo aliyeonekana bado alikuwa yupo bwi kwa kilevi kuteremka katika daladala akitokea Buguruni.

“Nahisi yule msichana ni dada poa na muda ule alikuwa akitokea kazini Buguruni, sasa vijana walipomuona alivyokuwa amevaa kipensi wakaanza kumbashia na kumzomea, isingekuwa dereva teksi mmoja kumkimbiza angefanyiwa kitu mbaya,” alisema shuhuda wa tukio hilo.

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini