Polisi wampiga vibaya Mwandishi wa Habari Zanzibar

Mwandishi wa Habari kwa jina Omar Ali mzaliwa wa Mkoani Kangani kisiwani Pemba, jana mida ya asubuhi ameshambuliwa na kupigwa vibaya sana na jeshi la Polisi Zanzibar na kutupwa maeneo ya Maisara mjini Zanzibar.

Mwandishi huyu alikuwa anachukua habari kutoka kituo cha uandikishaji dafatari la kudumu maeneo ya Migombani Zanzibar na polisi hao inasadikiwa walisema ni mwandishi wa Chama cha Wananchi CUF na ndipo walipomshika na kuanza kumpiga vibaya sana na kumvunja miguu kama anavyoonekana kwenye picha akiwa hospital mahutui miguu ikiwa imevujika.

Ikumbukwe:
Matukio haya yanakuja baada ya wananchi wa Zanzibar kuhakikisha kila kituo hawezi kuandikishwa mtu ambaye hahusiki kama ambavyo tumeona na kuskia kupitia vyanzo mbali mbali mpango wa CCM kupeleka mamluki visiwani Zanzibar kujiandikisha kwaajili ya kukiokoa Chama cha Mapinduzi hasa Zanzibar ambako kuna kila dalili kungoka madarakani Oktoba mwaka huu.

Chanzo:http://www.udakuspecially.com

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini