MKUU WA MKOA WA MBEYA AIAGIZA SUMATRA KUANGALIA MIKATABA YA MADEREVA


NA KENNETH NGELESI,MBEYA
MKUU wa Mko wa Mbeya Abbas Kandoro ameiagiza Mamlaka ya Udhibiti na Usafiri wa  nchi kavu na majini (Sumatra) kuanza kukagua mikataba ya ajira kwa madereva kwani wengi wao hujiingiza katika vitendo hivyo ,hawana ajira na hufanya hivyo kama njia ya kuongeza vipato vyao.

Kandoro amefikia hatua ya kutoa agizo hili ikiwa ni  siku  tatu baada ya kuzinduliwa wiki ya usalama barabarani, siri ya kukithiri kwa ajali akisema kuwa kuna mawakala wanaokatisha tiketi katika vituo vya mabasi  huwalipa motisha ya fedha madereva  ili wawahi kufika mapema, hali inayochochea ongezeko la ajali hizo nchini.

Akizungumza katika kipindi cha tuongee asubuhi, habari kuu, kinachorushwa na kituo cha televisheni cha Star Tv cha Jijini Mwanza, Kandoro alisema  kwamba mawakala hao wamekuwa wakitoa fedha hizo kwa madereva wakiamani kuwa gari likifika mapema katika vituo litakuwa likipendwa na abiria.

Alisema kuwa utafiti tulioufanywa katika vituo vya mabasi  katika majiji la Mbeya na  Dar es salaam unaonesha kuwa kuna mawakala wanaokatisha tiketi huwapa motisha ya fedha madereva (maarufu kwa jila la day waka) kwa  kwanawapa motisha .

 ‘Kwasababu wanaamini kuwa gari inayofika mapema inaonekana miongoni mwa abiria kuwa ni gari inayoaminika, imara  inayoweza kuwafanya wafanikishe  kusafiri kwa haraka  na kuwahi shughuli zao za biashara” alisema Kandoro.

Hata hivyo, alisema vitendo hivyo havikubaliki na kuwataka wananchi na wadau wa usafiri nchini kutoa taarifa  za siri ili kuwafichua watu hao wanaoendekeza vitendo hivyo vinavyohatarisha na kugharimu maisha ya watanzania .

Kuhusu agizo la Sumatra kukagua mikataba ya madereva, Kandoro alisema kuwa hali hiyo inaweza  kwa kiasi kikubwa kuwadhibiti wa wamiliki wa magari  kuacha tabia iliyozoeleka ya kuifanya sekta ya usafirishaji ya holela na kusababisha madereva kufanya mambo ya hovyo yanayohatarisha maisha ya watu.

Kandoro alisema kuanzia Januari hadi Septemba 10 mwaka huu jumla ya ajali  kwa mwaka huu kuanzia Septemba jumla ya ajali 297 zilitokea mkoani Mbeya na kusababisha vifo vya watu 210, huku majeruhi ambao baadhi yao wamepata ulemavu wa kudumu wakiwa 402.

“Sasa hali inaonekana kama haitachukuliwa jitihada za makusudi kudhibiti mambo yatakuwa mabaya zaidi, kwani ndani ya mwezi huu wa Septemba pekee  jumla ya ajali  zilizotokea ni 16 na kusababisha vifo 11 na majeruhi 15” alisema Kandoro.

Wiki iliyopita Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Kandoro alifanya ziara ya kushtukiza majira ya saa 11:00 alfajiri katika kituo kikuu cha mabasi Mbeya na kuzungumza na abiria, madereva , mawakala wa kukatisha tiketi  na wapiga debe akiwaasa kufuata taratibu ili kuthibiti wimbi la ajali.

Hata hivyo kauli hiyo ya Kandoro imekuja ikiwa siku chache tangu Mwenyekiti wa chama cha madereva wa mikoani (TDA), Protas Mpora, alisema  changamoto nyingine inayochangia  ongezeko la ajali ni madereva wengi kutokuwa na sifa kutokana mfumo wa sekta hiyo kutokuwa na mfumo mzuri.

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini