Arsene Wenger: Alexis Sanchez na Luis Suarez ni wapiganaji


Arsene Wenger anaamini wawili hao ni maalumu kutokana na machimbuko yao ya utotoni huko Amerika Kusini.

Kocha wa Arsenal Arsene Wenger anasisitiza kuwa upambanaji unaopnyeshwa na Alexis Sanchez na Luis Suarez umetengenezwa na mitaa ya Amerika Kusini.
Wenger anahusudu nguvu na bidii ya mchezaji wa Chile Sanchez, ambaye Gunners walimsajili msimu huu kwa ada ya pauni milioni 35 kutoka Barcelona.
Mfaransa huyo anaamini utawala wa washambuliaji wa Latini Amerika katika soka la Ulaya ni matokeo ya malengo wanayohitaji kuyafanikisha katika nchi zao, huku mataifa yaliyoendelea wamekuwa laini.

Alexis Sanchez amekuwa na roho ya kupambana ambayo Arsenal waliikosa kwa misimu ya hivi karibuni.


“Tazama Ulaya nzima ni wapi wanatoka washambuliaji? Wengi wao, karibia asilimia 80, wanatoka Amerika ya Kusini,” alisema Wenger.
“Labda kwa sababu soka la mitaani Ulaya limekufa. Soka la mtaani, ukiwa na miaka 10, unataka kuja kucheza ukiwa na miaka 15.


Sanchez amekuwa akiisaidia Arsenal kufanya vizuri katika msimu huu, akiwa amefunga magoli 15 mpaka sasa.


“Kisha unatakiwa kudhihirisha kuwa umzuri, unapambana na kushinda mipira isiyowezekana.
“Lakini si kila Mmarekani wa kusini ana hilo, ukirudi miaka 30 au 40 nyuma nchini England, maisha yalikuwa magumu.
“Ila kwa sasa jamii imebadilika. Tumekuwa watu wa kujihami zaidi ya ilivyokuwa miaka 20 au 30 iliyopita. Tumekuwa walaini kidogo.

Luis Suarez wa Barcelona maarufu kwa mpira wa kibabe uwanjani.
“Ukiona mahali wanakotoka, mahali alipozaliwa, na kasha anacheza Barcelona au Arsenal, lazima awe na kitu maalum.

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini