RAIS NKURUNZIZA AWAFUTA BAADHI YA VIGOGO KWENYE NYADHIFA ZAO

Na RFI
Rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza amewafuta washirika wake wa karibu kwenye nyadhifa zao.
Mkurugenzi kwenye afisi ya rais jenerali Alain-Guillaume Bunyoni na mkuu wa Idara ya Ujasusi jenerali Adolphe Nshimirimana ambao wamekua na ushawishi mkubwa kwenye utawala wa Pierre Nkurunziza, wameondolewa kwenye nyadhifa zao.
Si hao tu, maafisa wengine waandamizi wamefutwa kwenye nyadhifa zao, ikiwa ni pamoja na wakurugenzi wawili kwenye afisi ya rais. Maafisa hao waandamizi wanadaiwa kuwa miongoni mwa vigogo wenye ushawishi mkubwa kwenye utawala.(P.T)
Uamzi huu ambao umewashangaza wengi, umetolewa baada ya kufanyika vikao vya siri. Hakuna mtu ambaye angelifikiri kuwa hali hii ingelitokea. Jenerali Alain Guillaume Bunyoni, ambaye ni miongoni mwa vigogo hao katika utawala wa Cndd-Fdd amekabidhi madaraka leo Ijumaa asubuhi, na nafasi yake imechukuliwa na raia wa kawaida. Kwa sasa Bunyoni ni katibu mtendaji wa Baraza la usalama wa taifa. amekua kama amewekwa kapuni.
Jenerali Adolphe Nshimirimana mkuu wa Idara ya Ujasusi, ambaye aliwahi kua mkuu wa majeshi wakati walipokua bado msituni na ambaye amekua akiendesha ukaguzi katika sekta nzima ya usalama, ameondolewa kwenye wadhifa wake, nafasi hiyo imechukuliwa na mkuu wa zamani wa majeshi, jenerali Godfroid Niyombare.
Maafisa wengine waandamizi ambao wana ushawishi mkubwa kwenye utawalawa Cndd-Fdd wamefutwa kwenye nyadhifa zao. Hali hii inatokea baada ya hali ya sintofahamu kuripotiwa katika uongozi wa juu wa maafisa wa kijeshi kutoka waasi wa zamani wa Cndd-Fdd. hata hivo, inaarifiwa kuwa sakata hilo bado linaendela.

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini