David De Gea ampiku Di Maria, atwaa tuzo United

Katika kura zilizopigwa na mashabiki wa The Red Devil, asilimia 70 ya kura zote zilimchagua kipa namba moja wa klabu hiyo, David de gea 23, kama mchezaji bora wa mwezi katika kikosi hicho.
Baadhi ya mechi zilizomzolea sifa kubwa Mhispania huyo ni pamoja na mechi dhidi ya West Brom,
Everton, na mechi dhidi ya Chelsea pale alipookoa michomo mingi ya wazi ikiwa ni pamoja na ule uliopigwa na Eden Hazard katika mchezo
moja kati ya mikwaju mingi iliyookolewa na De Gea katika mechi dhidi ya Everton
ulioishia kwa suluhu ya 1-1.
David de gea  akiokoa shuti lililopigwa na Eden Hazard katika mchezo dhidi ya Chelsea ulioishia kwa sare ya 1-1 katika uwanja wa Old traford.
Katika mwendelezo wa mbio za kuwania ubigwa wa ligi kuu nchini Uingereza,
klabu ya Manchester City itawakaribisha watani wao wa jadi Manchester United katika dimba la Etihad  kesho Jumapili ya tarehe 2 Novemba,
kikosi cha Man City kina hatihati ya kuwakosa David Silva pamoja na Yaya Toure waliopata majeraha katika mechi ya kombe la FA dhidi ya Newcastle.

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini