Ulikosa Habari kubwa za ITV, ziko hapa. Ipo taarifa ya Escrow, ajali ya basi iliyoua na Mahakama ya watoto

Walichokisema Wananchi kuhusu ishu ya Ripoti ya Escrow
Baada ya Ripoti ya PAC kusomwa Bungeni na Bunge kuanza kuijadili Ripoti hiyo watu mbalimbali wameonekana kusikitishwa na jinsi hali ilivyo ambapo mpaka baadhi ya viongozi wa kidini wametajwa kuhusika katika mgao wa pesa zilizochotwa kutoka kwenye akaunti ya Escrow.
Mmoja kati ya wananchi hao amesema; “… Sijui ni Mungu gani ambaye wao wanamuabudu, yaani kama wangepata nafasi japo ya dakika moja kuchungulia wananchi tunapata shida kiasi gani wasingefanya mambo wanayoyafanya. Nimesikia kwamba kuna viongozi wa dini wanaohusika kwenye suala kama hilo, nimesikia Mheshimiwa wetu Waziri Mkuu alikuwa anajua ishu nzima na hajawahi kuongea jambo lolote mpaka watu wamekuja kujua yeye ndio anaongea… nimejisikia vibaya na sijapenda…
Ajali ya basi la Tanga
Siku ya jana Novemba 27 imeripotiwa ajali mbaya ya barabarani ambapo gari aina ya Coaster iliyokuwa imepakia abiria ilipata ajali kwa kugongana na lori la mizigo eneo la Mkanyageni Tanga, ambapo watu 11 walifariki kutokana na ajali hiyo na wengine  majeruhi ni 25 ambapo chanzo cha ajali hiyo kimesemekana kuwa ni dereva lori kuyumba na kuigonga gari hiyo ya abiria.
UNICEF kujenga Mahakama ya watoto Mbeya
Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia watoto Duniani UNICEF limeahidi kusaidia ujenzi wa Mahakama ya watoto Mbeya kutokana na Mkoa huo kukidhi viwango vya uanzishwaji wa Mahakama hiyo ambapo hii itakuwa ni Mahakama ya pili kwa Tanzania, nyingine ikiwa ni Mahakama ya Kisutu Dar.
Mkoa huo umechaguliwa kutokana na kukidhi vigezo vya kuanzishwa Mahakama hiyo ambavyo ni pamoja na uwepo wa madawati ya jinsia na watoto katika vituo vya Polisi na pia uwepo wa Waendesha mashtaka na Mawakili wa Serikali wanaoshughulikia mashtaka ya watoto.

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini