AY: Wazungu wamenitibulia sapraizi



Ambwene Yesaya ‘AY ‘.

Gabriel ng’osha
Hii nayo kali! Unajua AY na ngoma yake iitwayo Zigo, sasa basi jamaa alifanya remix ya wimbo huo akimshirikisha Diamond kisha kutaka kufanya sapraizi kwa Wabongo.

Unajua kilichotokea? Unaambiwa Wazungu ambao ndiyo waliotengeneza kichupa cha wimbo huo wakawapiga picha kisha kuziachia mtandaoni, kitendo kilichotibua kila kitu.

“Nilitaka kufanya sapraizi kwa kufanya video ya wimbo huo kwa siri kisha kuja kuiachia kwa kuwashtukiza. Kumbe bwana Wazungu wametupiga picha bila sisi kujua na kuzitupia mitandaoni, yaani wametibua mambo mwanangu,” alisema AY.

ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini