Baada ya kumsimamisha kwa muda usiojulikana, Dec 28 Yanga yatangaza maamuzi magumu kwa Niyonzima …

Baada ya stori za muda mrefu kuhusu kiungo wa kimataifa wa Rwanda anayekipiga katika klabu ya Yanga Haruna Niyonzima, uongozi wa klabu hiyo December 28 umetangaza maamuzi mapya baada ya awali kutangaza kumsimamisha kwa muda usiojulikana kutokana na utovu wa nidhamu.

Yanga wamefikia maamuzi ya kuvunja mkataba na kiungo huyo, baada ya kukaa na kufikiria kwa kina kutokana na tabia ya kiungo huyo kuwa kila anapokwenda kwao kucheza timu yake ya taifa ya Rwanda, huwa anachelewa kurudi bila sababu za msingi na wala taarifa rasmi.


Baada ya Yanga kutangaza maamuzi hayo kwa kile wanachokidai kuwa mchezaji huyo ameshindwa kuheshimu mkataba wake, Yanga wanadai fidia ya dola 71000 kama fidia ya kuvunja kwa mkataba huo, kwani wanadai mwenye makosa ni Haruna Niyonzima. Kiungo huyo wa kimataifa wa Rwanda alikuwa na mkataba na Yanga hadi mwaka 2017.



CHANZO CHA HII STORI: Shaffihdauda.com

ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini