Man United na Chelsea zatoka sare, matokeo mengine yapo hapa





Ligi Kuu ya Wingereza jana usiku imeendelea kwa kuchezwa michezo nane katika viwanja tofauti huku mchezo mkubwa uliokuwa unasubiriwa kwa hamu ni kati ya Manchester United na Chelsea mchezo uliochezwa katika uwanja wa Old Trafford.

Mchezo huo ulisubiriwa na wengi kutokana na hali zilizonazo timu hizo kwa sasa hivyo kuifanya dunia kusubiri mchezo huo kuona nani ataweza kumshinda mwenzake lakini mchezo huo ukaishia kwa sare ya bila kufungana.

Manchester United kama kawaida yao walimiliki mpira kwa muda mwingi wa mchezo huo lakini ikawa na shida katika kumalizia pasi za mwisho huku Chelsea wakionekana kucheza kwa tahadhari wakimwacha mbele Eden Hazard ambaye alionekana kuwa na usumbufu katika eneo la Manchester United.

Timu zote zilikuwa zikishambuliana kwa zamu lakini hadi dakika 90 zinamalizika hakuna aliyefanikiwa kuingia katika nyavu za mwenzake.

Matokeo mengine ya michezo ya jana;

Manchester United 0 – 0 Chelsea

Crystal Palace 0 – 0 Swansea

Everton 3 – 4 Stoke City

Norwich 2 – 0 Aston Villa

Watford 1 – 2 Tottenham Hotspur

West Bromwich Albion 1 – 0 Newcastle United

Arsenal 2 – 0 AFC Bournemouth

West Ham United 2 – 1 Southampton


ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini