Shilole mpaka Nigeria? kayazungumza haya kuhusu collabo aliyoifanya na msanii wa Nigeria…

Headlines za Dec 28 zinakwenda kwa Shilole ambaye wiki kadhaa zilizopita alikuwa nchini Nigeria kwaajili ya show yake akiwa na Feza Kessy & Lina Sanga, sasa msanii huyo baada ya kurudi Tanzania amefanya exclusive interview na ripota wa millardayo.com kufunguka kuhusu collabo aliyoifanya nchini Nigeria.


‘Nilikuwa niko Nigeria kwaajili ya kufanya show na kutafuta connection ya muziki wangu na nimepata bahati ya kufanya collabo na msanii mkubwa ambaye pia ni producer wa Nigeria anaitwa Selebobo aliyetengeneza hit single mpya ya Yemi Alade ‘Na Gobe (Swahili Version)’ na nyinginezo….hiyo single niliyofanya na Selebobo ndio itakuwa single yangu mpya itakayofuata ..kwa hiyo mashabiki wakae mkao wa kuisubiri inshallah Mungu akijaali nitaitoa mwakani’>>>Shilole

Unaweza ukabonyeza Play kumtazama Selebobo akiimba wimbo wake unaoitwa Selfie


ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini