WAZIRI WA UJENZI,UCHUKUZI NA MAWASILIANO AONGEA NA MENEJIMENTI YA ILIYOKUWA WIZARA YA UCHUKUZI NA KUTEMBELEA BANDARI

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, akisisitiza jambo wakati alipokutana na Menejimenti ya iliyokuwa Wizara ya Uchukuzi, na wakuu wa Taasisi zilizo chini yake, katika Ofisi za Wizara hiyo leo asubuhi. Waziri Mbarawa amewasisitiza Viongozi hao kuwa waadilifu na kufanya kazi kwa kasi.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa (wa pili kutoka kulia) na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Eng. Edwin Ngonyani ( wa kwanza kutoka kulia), wakimsikiliza Bi. Mkami Chacha kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), wakati alipokuwa akiwaleza namna mashine ya Kukagua makontena inavyofanya kazi, leo mchana wakati Mawaziri hao walipotembelea Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kuona kazi mbalimbali zinazofanywa na Mamlaka hiyo.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Eng. Aloyce Matei akimwonyesha Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa (wa pili kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu) eneo itakapojengwa gati 13 na 14, wakati Waziri huyo alipotembelea Mamlaka hiyo leo Mchana.


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, akisisitiza jambo kwa wafanyakazi wa Taasisi mbalimbali wanaofanya kazi katika kituo cha pamoja (one stop center) katika Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) wakati alipowatembelea leo Mchana. Waziri Mbarawa amewasisitiza watumishi hao kufanya kazi kwa uadilifu.


ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini