Ndege ya abiria ilivyokatiza safari yake angani kisa Panya..




Matukio yameendelea kuchukua headlines India.. ukiachia lile tukio la joto kali lililofanya watu kushindwa kuvumilia na kukaa ndani ya maji wakihofia maisha yao huku wengine wakipoteza maisha kutokana na joto kali kuna hii nyingine imetokea huko.

Ndege ya Air India ambayo ilikua ikitoka Mumbai kuelekea London, Uingereza ililazimika kugeuza safari ikiwa na abiria wake 171 na kurudi ilipotoka baada ya abiria kubaini kuwepo kwa panya ndani ya ndege hiyo.

Ingawa juhudi za kumpata panya huyo ziligonga mwamba lakini rubani alilazimika kurudi Mumbai ili kuwatoa wasiwasi abiria zaidi ya 170 waliokuwa wakisafiri kwa kutumia ndege hiyo ya shirika la ndege la India.

Baada ya kutua abiria walilazimika kubadilishiwa ndege na kuanza safari upya ya kuelea London.


ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini