Rais MAGUFULI Ampinga Balozi SEFUE Live!

Makatibu wakuu na manaibu wao walifika Ikulu kwa ajili ya shughuli ya kuapishwa kushika nafasi zao na baadaye kusaini kiapo cha uadilifu kilichoongozwa na Naibu Kamishna wa Maadili, Waziri Kipacha.
Mara baada ya Kamishna huyo kusoma kiapo hicho kwa niaba ya makatibu wakuu na manaibu hao, Katibu Mkuu Kiongozi aliwataka makatibu wakuu na manaibu hao kila mmoja asaini katika hati aliyopewa.
Utaratibu huo uliotangazwa na Balozi Sefue ulionekana kutomridhisha Rais Magufuli ambaye katika hali ambayo haikutarajiwa, aliinuka kutoka sehemu aliyokuwa amekaa na kutoa utaratibu tofauti.
“Hapana huwezi kula kiapo kwa niaba ya mtu mwingine wakati wenyewe wote wapo hapa, kila mmoja aape kwa mdomo wake mwenyewe na kusaini," alisema Rais Magufuli na kutoa angalizo:
"Kama kuna mmoja wao hajakubalina na kifungu kwenye hati hii tutajuaje?
“Kama yupo Katibu Mkuu au Naibu Katibu Mkuu anayeona kuwa hataweza kutekeleza mojawapo ya vifungu vilichopo katika hati hiyo ya maadili akae pembeni atuache wengine tuendelee.”