CCM KIZUNGUMKUTI! RAFU ZATAWALA KURA ZA MAONI!

 Rafu zimetawala katika kampeni za kumtafuta mgombea wa CCM katika jimbo la Nyasa ambapo wagombea tisa kati ya kumi wamelalamikia rafu zinazofanywa na mgombea mwenzao ambaye pia ni mkuu wa mkoa wa Rukwa Bi.Stella Manyanya ikiwemo mgombea huyo kugawa kadi za CCM zaidi ya ya elfu saba kinyume na utaratibu huku akinadiwa na mkuu wa wilaya ya Nyasa Bi. Magret Malenga kinyume na utaratibu.

Kutokana na rafu hizo zikiwemo za kutoa rushwa na kugawa kadi kwa wanafunzi na kutoa lugha za kejeli dhidi yao wamesema wameamua kugoma huku wakitaka ufumbuzi wa suala hilo ufanyike.
Kwa upande wake kaimu katibu wa CCM wa wilaya ya Nyasa Bw. Mussa Mwevi amekiri kuwepo kwa saka ta la kuingizwa kadi kinyume na utaratibu na kwamba litashughulikiwa baada ya kupita kura za maoni Agosti moja.

Naye mkuu wa wilaya Nyasa Bi. Margaret Malenga amekana tuhuma za kumnadi Bi. Stela Manyanya huku Bi. Manyanya akisema sakata hilo la kadi na malalamiko mengine atalizungumza kwenye vikao vya chama cha mapinduzi.

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini