KAMA UPO JIJINI NA BADO HAUJAJIANDIKSHA BASI HII TAARIFA INAKUHUSU SANA MDAU!

11811510_1065246360159936_8140805964569826706_n
Mwenyekiti wa NEC, Jaji Mstaafu Damian Lubuva .
 Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema kuwa inaongeza muda wa siku nne tu wa kuandikisha wapiga kura kwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam. Hii inamaanisha kuwa zoezi hilo ambalo lilikuwa linaisha ijumaa ya kesho julai 31, litaendelea hadi jumanne agosti 4
 Akiongea na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa NEC, Jaji Mstaafu Damian Lubuva amesema kuwa hataweza kuongeza muda wa zaidi ya siku nne kwa kuwa ratiba zitaingiliana.
Aidha, Jaji Mstaafu Lubuva amesema mpaka sasa watu zaidi ya milioni 18 wameandikishwa katika daftari la kudumu la wapiga kura kwa njia ya mfumo wa kielektroniki BVR kwa nchi nzima.

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini