IKULU Sio Pango la Majambazi na Wezi

Kamwe huwezi ukasafisha haja kubwa ikawa safi hata ufanye nini. Kiwango cha kufika mpaka wakuu wa vyama kuhongwa na kuhongeka hii ni hatari sana.

Kuna mambo mengi ambayo tunashindwa kuyadadavua kwa umakini sana na kuyachukulia kiushabiki tu. Eti tukiwa na lengo lakung'oa chama fulani wakati hatujui hatima yetu itakuwa ni nini. Tunasema tumg'oe kwanza huyu halafu baadae tutaona cha kufanya. Ni ujinga uliopita mipaka na kuwafanya watanzania kama hamnazo.

Siasa za namna hii zinalifanya taifa letu lizidi kudidimia. Vyama vina maprofessa, na watu wenye elimu ya hali yajuu kabisa wanashindwa kuleta dira na kuanza kuwa na cheap politics. Kuwahadaa wananchi kwa lengo lao tu. Mtu alishachafuka tangu miaka ya 90 na nyie wenyewe mnalijua kabisa. Lengo lenu ni nini katika nchi hii? kamwe hamfai na hakika mtakaa kusubiri meli stand ya basi.

Sio kwamba hatuoni nyendo zenu, hakika tunaona. Mwizi na jambazi sugu akabidhiwe nchi je atawalipa nini wafadhili wake waliompa pesa na kuweza kuwahonga viongozi wa vyama vya siasa? Huyu lazima analengo baya sana na nchi yetu.

Watanzania tusimame kwa pamoja tuwakatae hawa wezi. Unajijua wewe ni mchafu na umechafuka kwani ni wewe tu unayeweza kuwa kiongozi wa nchi hii? Unalengo gani na Tanzania? Unajinadi wewe ni mtu wa mungu!! wewe wewe wewe jichunguze usiwadangaye wananchi. eti unasema wewe prezidaa mmetoka mbali, aibu sana. Hutakiwi kuwa kiongozi wa tanzania wewe kaa utulie upate penshen yako kwa faida yako na kizazi chako.
Tukutane na wewe 25 October 2015 utauona moto wetu. Isitoshe report ya uchunguzi ipo tayari 

-JF

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini