Facebook Vs Instagram nani ana watumiaji wengi zaidi duniani? Majibu yake haya hapa.





Kama wewe ni miongoni mwa wale watu wanaohisi Facebook ni mtandao uliopitwa na wakati, basi utapendaa kusikia taarifa hii.

Mwishoni mwa mwezi wa sita kampuni ya FB Tech30 ama Facebook ilitajwa kuwa na watumiaji takribani bilion 1.5 kwa mwezi tu, watu wanaoutumia mtandao wa Facebookduniani kwa mwezi tu unazidi matumizi ya mitandao mengine duniani kama Microsoft(MSFT Tech30).


Ukuaji wa namna hii umeiruhusu Facebook kubuni features tofauti ili kuwezesha kampuni hiyo kukusanya data na taarifa tofauti za watumiaji wa mtandao huo.

Licha ya hayo ofa ya matangazo yanyotolewa na Facebook imewaingizia kampuni hiyo zaidi ya dola Bil 3.8 ambalo ni ongezeko la 43% ya ukuaji wao toka mwaka jana…Ofa ya matangazo ya facebook kupitia simu za mkononi inawaingizia zaidi ya dola Bil 2.9 na zaidi ya 62% ya mapato ndani ya miaka 3.


Facebook imeendelea kukua na kwa sasa imeweza kuwapiga gepu washindani wake wakubwa kama Twitter (TWTR, Tech30). Jumanne ya wiki hii Interim CEO wa TwitterJack Dorsey alisema kuwa ukuaji wa Twitter umekuwa ukishuka kwasababu watu wengi hawaelewi kwanini wanahitaji kuutumia mtandao huo.


Mwanzilishi na Mkurugenzi wa mtandao wa Facebook, Mark Zuckerberg amesema kuwa mafanikio makubwa ya mtandao huo ni dhamiria rahisi ya kuelewa namna ya kurahisisha mawasiliano na wanajitahidi kukuza na kusupport vitu vinavyo ibeba dhamira hiyo.


Licha ya Instagram kuwa maarufu sana kwa matumizi ya watu wengi siku hizi idadi ya watumiaji wa mtandao huo ni 26% duniani wakati idadi ya watumiaji wa Facebook duniani ni 71% na kwa zaidi ya miaka 3 iliopita wamekuwa product ya teknolojia inayotumiwa zaidi duniani.

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini