Iringa walalamikia wagombea kuwaomba kura vilabuni wakinywa pombe

Wananchi wa vijiji vya  Mufindi Kaskazini wamelalamikia baadhi ya  wagombea wa vyama vya siasa kufanya kampeni zao za kuomba kura kwenye  vilabu vya pombe za kienyeji.
Vijiji vya Mufindi Kaskazini ni ukelemi, Uyele, Saadani, Mbugi,  Tambalangíombe, Uhambila, Lugoda, Mapogolo pamoja na Ikweha.
 
Akizungumza na waandishi wa habari mmoja wa wakazi wa kitongoji cha  Ulaya kijiji cha Ikwea, Lutego Blastus, alisema toka zimeanza kampeni  hawajawahi kuwaona wagombea wa vyama vya siasa kufanya kampeni zao,  lakini kuna mgombea mmoja wa udiwani kupitia Chama cha Demokrasia na  Maendeleo(Chadema), alikwenda kufanya kampeni kwenye klabu cha pombe.
 
Sisi wanakijiji tunaomba wawe wanakuja kufanya kampeni zao kwenye  sehemu zenye viwanja maana mtu akifanya kampeni kwenye kilabu anakuwa  kama anatudanganya maana wakati huo tunakuwa tumelewa,î alisema.
 
Naye, Elimas Waya, alisema wanawaomba wagombea waende kufanya kampeni  kwenye kijiji chao kwani tangu zilipoanza wamemuona mgombea huyo  mmoja tu ambaye alienda kufanya kampeni kwenye klabu.
 
Pia wanakijiji hicho walisema pamoja kutowaona wagombea wa vyama  vingine kufanya mikutano kwenye kijiji chao bado wataendelea kumuenzi  Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwa kuhakikisha wanachagua  viongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM).
 
Waya alisema kuwa bado hajaona matatizo ya CCM ndio maana katika  kijiji chao hawapendi kusikia vyama vingine huku akiwataka  wanasiasa  hao waache kupotosha watu wakiwa wamelewa na kwamba kama wanataka  kufanya kampeni ni vyema wakafuata utaratibu waliopangiwa.

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini