PICHAZ: SHUHUDIA DK MAGUFULI ALIVYOFANYA IRINGA MJINI...WASANII WAFANYA YAO KAMA KAWA, KAMA DAWA!

Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk. John Magufuli akijinadi kwa Wananchi wakati wa mkutano wa kampeni kwenye Uwanja wa Samora, mjini Iringa.
 Mjumbe wa Kamati ya Kampeni za CCM, William Lukuvi akitangaza wasifu wa mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk Magufuli wakati wa mkutano wa kampeni kwenye Uwanja Samora mjini Iringa.
 Nape Nnauye akiwaomba wananchi kumuombea afya Mgombea urais  kupitia Chadema, Edward Lowassa ili aje ashuhudie CCM ikishinda urais.
 Dk Magufuli akimkabidhi Ilani ya Uchaguzi ya CCM Mgombea ubunge Jimbo la Iringa, Frederick Mwakalebela wakati wa mkutano wa kampeni mjini Kilolo, Iringa
 Dk Magufuli akimnadi mgombea ubunge Jimbo la KIalenga kupitia CCM,  Mgimwa wakati wa mkutano wa kampeni katika Mji wa Ifunda.
Dk Magufuli akipokea kadi za watu waliojiunga na CCM baada ya kuvihama vyama vyao jana mjni Ilula.
mwana FA akikamua iringa mjini.
Khadija Kopa, akifanya yake Iringa mjini.
Temba na chegge wakikamua iringa mjini.
Frederick Mwakalebela na MwanaFA wakipiga push up kuonesha kuwa wako fiti.
wakazi wa Ilula wakimsikiliza magufuli.
Mgombea urais kwa tiketi ya CCM. Dk. John Pombe Magufuli jana aliendelea kupiga kampeni za kuomba kura za urais pamoja na wabunge na madiwani wake.
Akiwa mkoani Iringa Magufuli alifanya mikutano mikubwa katika miji midogo ya Ifunda, Irula na kisha alimalizia kwa mkutano wa mwisho uliofanyika uwanja wa Samora uliopo Iringa mjini. Akiwa Iringa mjini Magufuli aliwanadi wagombea wake akiwemo Frederick Mwakalebela  anayegombea jimbo la Iringa mjini.
(Habari/Picha: Richard Bukos)

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini