Selfie Nyingine Iliyosababisha Kifo Cha Mwanafunzi Huyu....[PICHAZ]

Bado matukio ya watu kupoteza maisha kutokana na upigaji wa picha za Selfie yameendelea kuripotiwa kila siku.
Hii nyingine ni mwendelezo wa matukio hayo ambapo huko Russia kuna mwanafunzi mmoja kawachukua marafiki zake na kutaka wamsindikize kwenda kupiga selfie ya kipekee kwenye moja ya majengo marefu nchini humo. 

Walipofika mwanafunzi huyo akapanda juu ya jengo hilo lenye gorofa tisa na akaanza kupiga picha ili atimize lengo lake la kupiga selfie ya kipekee.
selfie
Sekunde chache baadaye aliteleza na kudondoka chini ambapo alikimbizwa hospitali akiwa na majeraha makubwa na baada ya masaa mawili kupita alifariki dunia.
selfie3

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini