Tetesi: Hali si Shwari Lumumba, Timu ya Kampeni ya Dr MAGUFULI Imeingiwa na Kiwewe cha Kushindwa!

Hali si shwari Lumumba timu ya kampeni ya Dr Magufuli imeingiwa na kiwewe cha kushindwa.
Baada ya Dr Pombe Magufuli kuzidiwa katika kampeni zinazoendelea viongozi wa kampeni wakiongozwa na Col Kinana wameanza kuparurana huku muda wa kampeni ukizidi kuyoyoma.Mnyetishaji anazidi kufunguka baadhi ya wapiga debe wameondolewa baada ya kubainika uwepo wao kunazidi kuiangamiza matumaini ya Dr Magufuli ya kuingia Ikulu ya magogoni.

Mikutano ya Dr Pombe hasa ule wa Mbeya na Iringa kumeondoa uwezekano wa kupata 25% ya kura.Wananchi wamechoka na wameonyesha hisia zao mbele ya mgombea.Wakuu wa mipango wamewaza na kuwazua mbinu zote zimeshindwa ikiwemo ya RICHMOND na Ugonjwa wa mgombea wa UKAWA zimeshindwa kumsaidia Dr Pombe.Tayari baadhi ya wapiga debe wameanza kujiandaa kushindwa na wengine wapo mbioni kuitosha CCM muda wowote kuanzia sasa.
Mikutano ya mgombea wa UKAWA Tanga na Mtwara mikoa ambayo miaka yote ilikuwa ndio ngome ya CCM sasa imegeuka na kukitosa CCM jambo ambalo limemfanya Mwenyekiti wa CCM kufuta safari zote alizotegemea kuzifanya kabla ya kuachia madaraka kwa kisingizio cha kwenda kuaga.Mikutano isiyokwisha imekuwa ikifanyika bila kuwa na majibu ya uhakika.Col Kinana na genge zima la kampeni wamechanganyikiwa.

Taarifa zaidi zinadai timu ya wazee iliyotumwa kwa Prof Mwandosya imeshindwa kumshawishi.Prof Mwandosya kanuna hataki kushiriki katika kampeni za Dr Magufuli.
Source: Ngongo/Jamii Forums

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini