FAHAMU UKWELII KUHUSU UGONJWA WA EBOLA

Ugonjwa wa Ebola unasababishwa na Virusi na ni ugonjwa hatari unaoambukiza haraka binadamu na wanyama mwitu (hayawani) kama kima, sokwe, popo, ndege, mijusi, amfibia, na kadhalika. Ugonjwa huu unaosababishwa na virusi aina ya Ebola Virus ni wa mlipuko.
Japokuwa hakuna mazingira maalum ambamo virusi vya Ebola vinapatikana, lakini wataalamu wanasema virusi hivyo vinapatikana kwa mnyama ambaye anapatikana zaidi barani Afrika.
Mlipuko wa Ugonjwa wa Ebola umetokea katika nchi nyingi na bado unaendelea kupukutisha maisha ya watu wengi hasa barani Afrika. Matukio ambayo yamethibitishwa kuwepo kwa ugonjwa huo ni katika nchi za Liberia, Sierra Leone, Guinea, Ghana, Nigeria, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Gabon, Sudan, Ivory Coast, Uganda na kadhalika.

 
Ugonjwa wa Ebola daima unasambaa ndani ya maeneo ya utoaji wa huduma za afya.Hata hivyo, matukio mengine yamekuwa yakitokea nje ya maeneo hayo na hayafahamiki.
Jinsi ugonjwa huo unavyosambaa:
Namna ugonjwa huo ulivyojulikana kwa mara ya kwanza hakuna anayefahamu kwa hakika. Hata hivyo, ugonjwa wa Ebola unaweza kusambazwa kwa njia zifuatazo:
1. Kugusana moja kwa moja na mtu ama mnyama mwenye ugonjwa huo;

2. Kugusana moja kwa moja na damu ama majimaji (mate au mafua) ya mtu mwenye ugonjwa huo katika familia;

3. Kugusa vifaa vya tiba vilivyo na virusi vya ugonjwa huo kama sindano;

4. Kutumia vifaa visivyochemshwa katika hospitali kama sinano;

5. Kula ama kushika vinyesi vya wanyama wenye ugonjwa huo;
6. Kuvuta hewa yenye virusi vya ugonjwa huo katika mazingira ya hospitali;
7. Kutumia nyama ya wanyama walioathirika kama kitoweo;
8. Kutozingatia tahadhari za kitaalam.

Dalili za Ebola:
Mtu au mnyama mpaka aonyeshe dalili za ugonjwa wa Ebola huchukua kati ya siku 2 hadi 21. Dalili za ugonjwa huo ni pamoja na:
1. Homa kali
2. Kuumwa kichwa

3. Kuharisha

4. Kutapika

5. Maumivu ya kifua

6. Maumivu ya tumbo
7. Mafua
8. Kikohozi
9. Maumivu ya misuli na viungo, hasa kwenye viungio
10. Kuvimba koo
11. Mwili kuwa dhaifu
12. Mfadhaiko
13. Kuchanganyikiwa
14. Macho kuwa mekundu
15. Kuvuja damu kwa ndani na nje

Nani aliye katika hatari?
1. Watu wanaofuga wanyama mwitu ama wanaoishi katika maeneo yenye wanyama mwitu;

2. Watu wanaotegemea wanyama mwitu kama popo kama chakula chao;

3. Watumishi wa vyumba ya kuhifadhia maiti;

4. Watumishi wa afya wanaowahudumia wagonjwa wa Ebola;

5. Watumishi wa afya katika hospitali ambazo hazina mazingira bora na safi;
6. Wanafamilia wa wagonjwa wa Ebola;
7. Watu wanaohudhuria hospitali ambazo hazina mazingira safi na salama;

Jinsi ya kujikinga na ugonjwa wa Ebola:
1. Epuka kugusa damu/majimaji ya wanyama ama binadamu walio na ugonjwa wa Ebola au hata maiti za watu waliokufa kwa ugonjwa huo kwa kuzingatia haya:
a) Tunza mazingira safi na salama ya hospitali;

b) Watelekeze wagonjwa wa Ebola;

c) Fukia miili ya waliokufa kwa Ebola kwa usalama;

d) Epuka mazishi ya kienyeji kama kuosha maiti za watu waliokufa kwa Ebola;

2. Watumishi wa afya na wanaowatazama wagonjwa wa Ebola wanatakiwa:
a) Kuvaa kwa usahihi vifaa vya kujikinga na nyuso, mikono na macho,

b) Na majoho maalum daima;

c) Kutumia sindano mara moja na kuziteketeza ama kuzifukia;

d) Epuka kutumia zaidi ya mara moja sindano au kutotumia sindano ambazo hazijachemshwa vyema;

e) Epuka kuosha maiti za watu waliokufa kwa Ebola;
CHANZO : BROTHER DANY BLOG

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini