Hiki ndicho walichoamua Mahakama kuhusu Chid Benz

Chid Benz leo mchana wa Oktoba 28 amesimamishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kusomewa mashtaka yanayomkabili.
Mashtaka hayo ni;
1.Kukutwa na madawa na vifaa vya kutayarishaji uvutaji wa madawa
2.Kusafirisha madawa ya kulevya
3.Utumiaji wa madawa ya kulevya
Kwa sasa Chidi Benz amerudishwa rumande hadi Novemba 11 ambapo kesi yake itatajwa tena, kuhusu dhamana itakuwa wazi kwa masharti ya kuwa na wadhamini wawili wanaoeleweka na jumla ya pesa taslim million 1.

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini